Kimbunga Pomboo chasababisha kunyesha mvua kubwa katika maeneo mbalimbali nchini China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Agosti 11, 2026
Kimbunga Pomboo chasababisha kunyesha mvua kubwa katika maeneo mbalimbali nchini China
Picha iliyopigwa Agosti 10, 2026 ikionyesha mashine ikifanya kazi ya dharura ya kuondoa udongo na mawe kwenye barabara ya mlimani iliyozibwa na maporomoko ya ardhi katika Wilaya ya Yongjia, huko Wenzhou, Mkoa wa Zhejiang, mashariki mwa China. (Xinhua/Jiang Han)

BEIJING – Kituo cha hali ya hewa cha kitaifa cha China kimetoa utabiri kikisema kuwa, kimbunga Pomboo kinaelekea ndani ya mikoa ya bara baada ya kutua katika sehemu mbili kando ya pwani ya Mkoa wa Zhejiang mashariki mwa China na kinatazamiwa kuleta mvua kubwa katika maeneo zaidi ya 10 ya mikoa.

Kituo hicho kimetoa tahadhari ya kimbunga ya rangi ya bluu jana Jumatatu asubuhi, kikitabiri mvua kubwa kunyesha kwa mfululizo hadi Jumatano katika mikoa ya Zhejiang, Jiangsu, Henan na Hebei. Baadhi ya maeneo yanaweza kukumbwa na mvua kubwa, dhoruba za radi na upepo mkali.

Idara husika za serikali za mitaa katika maeneo mbalimbali zimefanya juhudi zote katika kuzuia mafuriko na kukabiliana na kimbunga hicho.

(Wahariri wa tovuti:Liu Mengxue,Zhao Jian)

Picha