Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang leo amesema China imetekeleza sera ya kufungua mlango kwa zaidi ya miaka 40, sera ambayo imeleta maendeleo kwa China na manufaa kwa dunia nzima, kwa hiyo China haitafunga mlango wake.
Waziri Mkuu wa China Li Keqiang akiitisha mkutano na waandishi wa habari Ijumaa baada ya ufungaji wa mkutano wa tano wa Bunge la Umma la 13 la China. Waziri Mkuu alijibu maswali ya waandishi wa habari wa ndani na nje ya China kwa kupitia video.