Viongozi waandamizi wa China jumapili walijumuika na washauri wa kisiasa wa taifa kwenye mijadala ya vikundi tofauti katika Mkutano wa tano wa Baraza la 13 la Mashauriano ya Kisiasa la China (CPPCC). Viongozi hao wakiwemo pamoja na waziri mkuu wa China Bw.
Rais Xi Jinping wa China Machi 7 mchana amewatembelea wajumbe kutoka sekta za kilimo, huduma za jamii, na bima za jamii wanaohudhuria kwenye Mkutano wa tano wa Baraza la 13 la Mashauriano ya Kisiasa la China. Pia rais Xi ameshiriki katika majadiliano kwenye kikundi cha wajumbe hao, na kusikiliza maoni na mapendekezo yao.
Ripoti ya kazi ya serikali ya China iliyotolewa tarehe 5 mjini Beijing imeeleza kuwa ni muhimu kupambana vikali na uhalifu wa usafirishaji haramu wa wanawake na watoto, na kulinda kwa uthabiti haki na maslahi halali ya wanawake na watoto. Ripoti ya kazi ya serikali pia imesema ni muhimu kuhakikisha watu wanaishi na kufanya kazi kwa amani na katika mazingira ya kuridhika, na kukuza utulivu wa jamii.
Ripoti ya kazi ya serikali ya China kwa mwaka 2022 iliyowasilishwa kwenye mkutano wa bunge la umma tarehe 5, imeeleza kutumia kikamilifu mitaji ya kigeni, na kufungua soko kubwa la China, jambo ambalo hakika litatoa fursa zaidi kwa makampuni kutoka nchi zote kujiendeleza nchini China. Ripoti hiyo imeeleza kuwa ni muhimu kupanua maeneo yanayoruhusiwa kuwekezwa na nchi za nje, na kuunga mkono mitaji ya kigeni kuwekezwa katika sera za uzalishaji wa hali ya juu na kati, utafiti na maendeleo, huduma za kisasa, na vile vile katika mikoa ya kati magharibi, na kaskazini mashariki.