(Picha inatoka CRI.) Mkutano wa 5 wa Bunge la Umma la 13 la China umefungwa baada ya kumaliza ajenda mbalimbali.
BEIJING - Wajumbe wa Bunge la Umma la 13 la China (NPC) walikuwa wamewasilisha mapendekezo 487 kufikia saa sita mchana siku ya Jumanne wiki hii, ambayo ni tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maoni na mapendekezo katika Mkutano wa Tano wa NPC ya 13 unaoendelea hapa Beijing, imesema sekretarieti ya mkutano huo. Sekretarieti hiyo imesema pia imepokea takriban maoni ya kiujenzi na ya kukosoa yapatayo 8,000, kutoka kwa wajumbe wa Bunge la Umma la China .
Wajumbe wa Bunge la Umma la China (NPC) na wajumbe wa Baraza la Mashauriano ya Kisiana la China (CPPCC) wakiendelea kufanya kazi zao za kawaida, pia wanajitahidi kuwasilisha maoni ya watu kwenye “Mikutano Mikuu Miwili” ya mwaka ya China. Juhudi zao za kubeba majukumu kadiri wawezavyo zinasifiwa sana na watu.
Mkutano wa 5 wa Baraza la 13 la Mashauriano ya Kisiasa la China umefungwa leo baada ya kumaliza ajenda mbalimbali kwa mafanikio. Viongozi wa Chama na serikali akiwemo rais Xi Jinping wamehudhuria ufungaji wa mkutano huo.