Zhao Leji, mwenyekiti mtendaji wa tume ya utendaji wa mkutano wa nne wa Bunge la 14 la Umma la China (NPC), akiongoza kikao cha pili cha tume hiyo ya utendaji wa mkutano katika Jumba la Mikutano ya Umma la Beijing, China, Machi 10, 2026. (Xinhua/Gao Jie) BEIJING – Tume ya Utendaji wa mkutano wa nne wa Bunge la 14 la Umma la China (NPC), imefanya kikao chake cha pili jana Jumanne, kikiongozwa na Zhao Leji, mwenyekiti mtendaji wa tume hiyo.
Kikao cha pili cha mkutano wa nne wa Bunge la 14 la Umma la China (NPC) kikifanyika kwenye Jumba la Mikutano ya Umma la Beijing, China, Machi 9, 2026. (Xinhua/Li Tao) BEIJING – Mkutano wa nne wa Bunge la 14 la Umma la China (NPC), chombo cha juu cha utungaji sheria cha China, umefanya kikao chake cha pili cha wajumbe wote jana Jumatatu.
BEIJING – Ripoti iliyotolewa jana Jumatatu kuhusu Kazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge la Umma la China (NPC), ambacho ni chombo cha juu cha utungaji wa sheria cha China, inaonesha kuwa, kamati hiyo ilihudumia na kuunga mkono mageuzi na maendeleo kwa kupitia utungaji wa sheria wa sifa bora katika mwaka uliopita. Ripoti hiyo ya kazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge la Umma la China iliwasilishwa jana Jumatatu kwenye mkutano wa nne bunge hilo la umma ili ithibitishwe.
Jana Tarehe 8 Machi ilikuwa Siku ya Wanawake Duniani. Kwenye mikutano mikuu miwili ya mwaka ya Bunge la Umma la China na Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China inayoendelea Beijing, wajumbe wanawake wanafanya kazi muhimu katika kuchangia hekima kwa maendeleo ya nchi.