Kituo cha Habari cha Mkutano wa Nne wa Bunge la Umma la 14 la China (NPC) na Mkutano wa Nne wa Baraza la 14 la Mashauriano ya Kisiasa la China (CPPCC), ambayo inafahamika kwa jina la “Mikutano Mikuu Miwili ya Mwaka ya China” kimefunguliwa rasmi leo Ijumaa mjini Beijing, na kinatarajiwa kutoa huduma kwa waandishi wa habari wa ndani na nje ya nchi watakaofuatilia. Mikutano hiyo inatarajiwa kuanza mjini Beijing Machi 5 na Machi 4, mtawaliwa.