“Kijiji No. 1 cha Mashua ya Dragon cha China” chawa na pilika za uzalishaji mashua wakati Sikukuu ya Duanwu ikiwadia (6)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Mei 26, 2025
“Kijiji No. 1 cha Mashua ya Dragon cha China” chawa na pilika za uzalishaji mashua wakati Sikukuu ya Duanwu ikiwadia
(Zhang Bin/ChinaNews)

Kijiji cha Fangzhuang, kinachopatikana katika Wilaya ya Minhou ya Mji wa Fuzhou, Mkoani Fujian, ni kijiji kikubwa zaidi kwa uundaji wa mashua ya dragon nchini China, kikiwa na historia zaidi ya miaka 700 ya uundaji mashua za dragoni.

Wakati inapowadia Sikukuu ya Duanwu, sikukuu ya China ambapo watu hufanya mashindano ya mashua ya dragon kwa ajili ya kuisherehekea, mafundi kwenye karakana ya uundaji mashua za dragoni ya kijiji hicho wana pilikapilika za kufanya kazi ili kuharakisha kumaliza oda za mashua za sikukuu hiyo.

Kwa mujibu watakwimu, kijiji hicho kwa sasa hupokea oda kwa zaidi ya mashua 200 kila mwaka, ambayo yana thamani ya jumla ya karibu Yuan milioni 6 (sawa na Dola za Marekani 836,466).

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha