Ukumbi wa Kuutazama Mji wa “Kilele cha Tianjin” wa China wafunguliwa rasmi kwa umma (2)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 23, 2025
Ukumbi wa Kuutazama Mji wa “Kilele cha Tianjin” wa China wafunguliwa rasmi kwa umma
Mtalii akijipiga picha kwenye Ukumbi wa Kuutazama Mji mzima wa “Kilele cha Tianjin” wa Kituo cha Mambo ya Kifedha cha Dunia cha Tianjin (TWFC) mjini Tianjin, kaskazini mwa China, Juni 22, 2025. (Xinhua/Sun Fanyue)

Ukumbi wa Kuutazama Mji mzima wa “Kilele cha Tianjin” kwenye ghorofa ya 79 ya Kituo cha Mambo ya Kifedha cha Dunia cha Tianjin (TWFC) mjini Tianjin, kaskazini mwa China kimefunguliwa rasmi kwa umma jana Jumapili ambapo watalii sasa wanaweza kufurahia mandhari ya mji huo wa Tianjin kutoka urefu wa mita 310.

Kikiwa kinapatikana kando ya Mto Haihe katika eneo la katikati mwa Mji wa Tianjin, Kituo hicho cha Mambo ya Kifedha cha Dunia cha Tianjin (TWFC) kinaelekea angani kwa hadi urefu wa mita 336.9, ikikifanya kuwa mojawapo ya majumba marefu zaidi ya mji huo tangu kukamilika kwake mwaka 2011. 

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha