Rais Xi Jinping ampongeza Jennifer Simons kwa kuchaguliwa kuwa rais wa Suriname

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Julai 14, 2025

BEIJING- Rais wa China Xi Jinping amempongeza Jennifer Simons kwa kuchaguliwa kuwa rais wa Suriname, na katika salamu zake za pongezi zilitozumwa Ijumaa, Rais Xi ameielezea Suriname ni mshirika wa China katika ushirikiano wa kimkakati katika eneo la Karibiani.

"Shukrani kwa juhudi za pamoja za pande zote mbili, uhusiano kati ya China na Suriname umefurahia ukuaji mzuri kwa hatua madhubuti, ushirikiano wa kufuata hali halisi umefanyika katika sekta mbalimbali na kupata matokeo yenye ufanisi mkubwa, na pande hizo zimefanya uratibu wa karibu katika mambo ya pande nyingi katika miaka 49 iliyopita tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia” Rais Xi amesema.

Amesema, anaweka umuhimu mkubwa sana kwenye ukuaji wa uhusiano kati ya China na Suriname na anapenda kushirikiana na rais mteule Simons katika kuzidisha ushirikiano wa kirafiki wa kunufaishana na kukuza zaidi ushirikiano wa kimkakati wa pande mbili ili kuleta manufaa zaidi kwa watu wa nchi hizo mbili.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha