Bandari ya mpakani mwa China na Mongolia yashuhudia kuongezeka kwa usafiri wa kuvuka mpaka (4)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Desemba 24, 2025
Bandari ya mpakani mwa China na Mongolia yashuhudia kuongezeka kwa usafiri wa kuvuka mpaka
Abiria akipita katika taratibu za ukaguzi wa mpakani kwenye bandari ya nchi kavu ya Erenhot, Mkoa Unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani, Kaskazini mwa China, Desemba 22, 2025. (Xinhua/Ma Jinrui)

ERENHOT - Erenhot, bandari kubwa zaidi ya nchi kavu kwenye mpaka wa China na Mongolia, ni sehemu muhimu ya Ushoroba wa Kiuchumi wa China-Mongolia-Russia.

Hadi kufikia Desemba 22, idadi ya abiria wanaoingia na kutoka na idadi ya magari yanayopita kwenye bandari hiyo ya nchi kavu ya Erenhot ilifikia milioni 2.753 na 741,000, mtawalia. Idadi hizo zimefikia ongezeko la asilimia 8.8 na asilimia 12.1 zikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha