Programu ya huduma za matibabu bila malipo inayosaidiwa na China yazinduliwa Zanzibar, Tanzania

(CRI Online) Januari 21, 2026

Wataalamu wa matibabu wa China jana Jumanne walizindua programu ya huduma za matibabu bila malipo ya "Timu 100 za Matibabu katika Vijiji 1,000" kwenye kituo cha huduma za afya ya jamii katika Kisiwa cha Pemba, Zanzibar, Tanzania.

Kampeni hiyo iliandaliwa kwa pamoja na timu ya wataalamu wa mradi wa kuzuia na kudhibiti kichocho Zanzibar unaosaidiwa na China na timu ya 35 ya madaktari wa China wanaosaidia Zanzibar, ikihusisha elimu ya afya ya kichocho na ushauri wa bure wa matibabu.

Kufuatia uzinduzi huo, wataalamu wa China walitoa elimu ya kuzuia kichocho na huduma za matibabu bila malipo kwa wakazi, ikiwa ni pamoja na upimaji wa afya, tathmini za hatari za kiafya, na ushauri kuhusu udhibiti wa magonjwa sugu na matumizi ya dawa.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha