Waandamanaji wakusanyika Tokyo kupinga ajenda hatari ya sera ya Waziri Mkuu Takaichi (4)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Februari 26, 2026
Waandamanaji wakusanyika Tokyo kupinga ajenda hatari ya sera ya Waziri Mkuu Takaichi
Mtu aliyeshikilia bango akihudhuria mkutano mbele ya Jengo la Ofisi ya Wajumbe la Pili la Baraza la Wawakilishi mjini Tokyo, Japan, Februari 24, 2026. (Xinhua/Jia Haocheng)

TOKYO - Umati mkubwa wa watu wa Japan walikusanyika Jumanne jioni mjini Tokyo kupinga msukumo wa hatari wa Waziri Mkuu Sanae Takaichi kwa sera zikiwemo za kuharakisha marekebisho ya katiba, kupanua uwezo wa kijeshi na kuimarisha kazi za ujasusi za taifa, wakielezea wasiwasi kuhusu mwelekeo wa siku za baadaye wa nchi hiyo.

Mkusanyiko huo wa umma, ulioandaliwa kwa pamoja na makundi kadhaa ya kiraia, ulikusanya watu mbele ya Jengo la Ofisi ya Wajumbe la Pili la Baraza la Wawakilishi. Washiriki walikuwa wameshikilia mabango yaliyoandikwa "Pinga marekebisho ya katiba" na "Usiachilie ufashisti kutoka kwenye kizimba chake," huku wakitamka kauli mbiu kama vile "Hapana Vita."

Noriko Kashikawa, mmoja wa waandamanaji hao, amewaambia waandishi wa habari kwamba kwa "asilimia 100 anapinga" ajenda ya sera ya Takaichi. Ameonya kwamba Japan inaelekezwa kwenye hali ya utayari wa vita wa kila mara, akisema kwamba kama nchi hiyo itaendeshwa kila wakati kuelekea migogoro, "hatimaye itapelekea kujiangamiza."

Kashikawa amesema Japan inapaswa kuzishinda changamoto kupitia mazungumzo na diplomasia badala ya kutunga sheria zinazozuia mawasiliano au kujenga mazingira ya msimamo mgumu wa nje.

Vijana wengi pia walionekana miongoni mwa umati huo. Mwanafunzi wa chuo kikuu anayeitwa Matsubara amesema ana wasiwasi na hatua za hivi karibuni za sera za serikali, akiongeza kwamba "sera hizi zote zinaonekana kuwa maandalizi ya kuanzisha vita." Ameelezea matumaini yake kwa serikali ambayo kwa usahihi zaidi inawakilisha sauti za umma.

Februari 20, Takaichi alisisitiza azma yake imara kwa marekebisho ya katiba wakati wa hotuba ya sera bungeni, akitoa wito wa kuimarishwa kimsingi kwa uwezo wa ulinzi wa Japan, upanuzi wa mauzo ya nje ya silaha hatari na kuongeza uwezo wa ujasusi wa taifa. Kauli zake hizo zimesababisha wasiwasi na ukosoaji mkubwa katika jumuiya mbalimbali za Wajapan. 

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha