Utalii wa kitamaduni wastawisha kijiji awali kilichokuwa maskini mkoani Guizhou, China (5)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) April 22, 2026
Utalii wa kitamaduni wastawisha kijiji awali kilichokuwa maskini mkoani Guizhou, China
Mtalii wa kigeni akitembelea Kijiji cha Kabila la Wadong cha Zhaoxing, Wilaya Liping, Mkoa wa Guizhou, kusini magharibi mwa China, Aprili 19, 2026. (Picha na Long Jianrui/Xinhua)

Kikiwa moja ya vijiji vikubwa zaidi vya China vinavyokaliwa na wakazi wa kabila la Wadong, Kijiji cha Kabila la Wadong cha Zhaoxing cha Wilaya Liping, Mkoa wa Guizhou, kusini magharibi mwa China hapo awali kilikuwa na maendeleo kidogo ya kiuchumi kutokana na usafiri duni na ukosefu wa sekta mbalimbali za kiuchumi.

Katika miaka ya hivi karibuni, kijiji hicho kimetumia kikamilifu nguvu bora za utamaduni wake wa kipekee wa kikabila na rasilimali za kiikolojia kuendeleza utalii wa kitamaduni, unaojumuisha maonyesho ya Wimbo Mkuu wa Kabila la Wadong, kujionea na kujaribu urithi wa utamaduni usioshikika, na nyumba za wageni na vyakula vya kienyeji.

Mwaka 2025, kijiji hicho kilipokea watalii zaidi ya milioni 1.51, na kuzalisha mapato kamili ya utalii yanayozidi yuan bilioni 1.5 (dola za Marekani karibu milioni 220.05), huku mapato ya pamoja ya kijiji yakizidi yuan milioni tatu (dola za Marekani karibu elfu 440.10).

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha