Lugha Nyingine
Utalii wa kitamaduni wastawisha kijiji awali kilichokuwa maskini mkoani Guizhou, China (7)
![]() |
| Picha iliyopigwa Aprili 20, 2026 ikionyesha mandhari ya Kijiji cha Kabila la Wadong cha Zhaoxing, Wilaya Liping, Mkoa wa Guizhou, kusini magharibi mwa China, Aprili 20, 2026. (Picha na Wu Guanghui/Xinhua) |
Kikiwa moja ya vijiji vikubwa zaidi vya China vinavyokaliwa na wakazi wa kabila la Wadong, Kijiji cha Kabila la Wadong cha Zhaoxing cha Wilaya Liping, Mkoa wa Guizhou, kusini magharibi mwa China hapo awali kilikuwa na maendeleo kidogo ya kiuchumi kutokana na usafiri duni na ukosefu wa sekta mbalimbali za kiuchumi.
Katika miaka ya hivi karibuni, kijiji hicho kimetumia kikamilifu nguvu bora za utamaduni wake wa kipekee wa kikabila na rasilimali za kiikolojia kuendeleza utalii wa kitamaduni, unaojumuisha maonyesho ya Wimbo Mkuu wa Kabila la Wadong, kujionea na kujaribu urithi wa utamaduni usioshikika, na nyumba za wageni na vyakula vya kienyeji.
Mwaka 2025, kijiji hicho kilipokea watalii zaidi ya milioni 1.51, na kuzalisha mapato kamili ya utalii yanayozidi yuan bilioni 1.5 (dola za Marekani karibu milioni 220.05), huku mapato ya pamoja ya kijiji yakizidi yuan milioni tatu (dola za Marekani karibu elfu 440.10).

Ndege wa Kwarara waingia msimu wa kuzaliana huko Shaanxi, China

Eneo la kaboni-sifuri katika Mkoa wa Hainan laonyesha vitendo vya kijani vya China

Vifaa vya kisasa vya usafi vyatoa huduma kwenye Mkutano wa Mwaka wa Jukwaa la Boao la Asia 2026

Eneo Jipya la Xiong'an la China labadilika kuwa mji wenye nguvu hai kutoka mpango
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
