Mfereji wa Pinglu mkoani Guanxi, China waingia katika maandalizi ya mwisho kwa ajili ya kufunguliwa Septemba (3)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 05, 2026
Mfereji wa Pinglu mkoani Guanxi, China waingia katika maandalizi ya mwisho kwa ajili ya kufunguliwa Septemba
Picha iliyopigwa Juni 3, 2026 ikionyesha maji yakisukumwa kuingia ndani ya kituo cha Qishi kwenye Mfereji wa Pinglu, Mkoa Unaojiendesha wa Kabila la Wazhuang wa Guangxi, kusini mwa China. (Picha na Zhao Zhenyu/Xinhua)

Maji yameanza kutiririka kupita sehemu kadhaa za mwisho za Mfereji wa Pinglu Jumatano wiki hii, na kuileta njia ya mkato ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu kukaribia kwa hatua moja kufunguliwa kwa usafirishaji wa kuelekea sehemu zilizoko kando za bahari za kusini mwa China.

Kwa kuwa maji yamesukumwa kwenye mfereji huo Jumatano asubuhi, njia hiyo ya maji yenye urefu wa kilomita 134.2 sasa imefikia muunganisho kamili wa mkondo na imeingia katika kipindi cha mwisho kabla ya uzinduzi wake unaotarajiwa mwezi Septemba.

Mfereji huo wa Pinglu ukianzia kutoka Mto Pingtang katika Mji wa Hengzhou, kupitia Mkoa Unaojiendesha wa Kabila la Wazhuang wa Guangxi, kusini mwa China, hadi Ghuba ya Beibu katika Bahari ya Kusini ya China, ni uti wa mgongo wa Ushoroba Mpya wa Biashara ya Kimataifa wa Baharini na Nchikavu wa China, mpango muhimu unaoongeza muunganisho wa biashara duniani na maeneo ya ndani ya bara ya magharibi mwa China.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha