Lugha Nyingine
Mfereji wa Pinglu mkoani Guanxi, China waingia katika maandalizi ya mwisho kwa ajili ya kufunguliwa Septemba (3)
Maji yameanza kutiririka kupita sehemu kadhaa za mwisho za Mfereji wa Pinglu Jumatano wiki hii, na kuileta njia ya mkato ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu kukaribia kwa hatua moja kufunguliwa kwa usafirishaji wa kuelekea sehemu zilizoko kando za bahari za kusini mwa China.
Kwa kuwa maji yamesukumwa kwenye mfereji huo Jumatano asubuhi, njia hiyo ya maji yenye urefu wa kilomita 134.2 sasa imefikia muunganisho kamili wa mkondo na imeingia katika kipindi cha mwisho kabla ya uzinduzi wake unaotarajiwa mwezi Septemba.
Mfereji huo wa Pinglu ukianzia kutoka Mto Pingtang katika Mji wa Hengzhou, kupitia Mkoa Unaojiendesha wa Kabila la Wazhuang wa Guangxi, kusini mwa China, hadi Ghuba ya Beibu katika Bahari ya Kusini ya China, ni uti wa mgongo wa Ushoroba Mpya wa Biashara ya Kimataifa wa Baharini na Nchikavu wa China, mpango muhimu unaoongeza muunganisho wa biashara duniani na maeneo ya ndani ya bara ya magharibi mwa China.

Meli kubwa ya kitalii ya pili kuundwa ndani ya China yakamilisha jaribio la kwanza la baharini

Hifadhi ya Taifa ya Kruger ya Afrika Kusini yaadhimisha miaka 100

Nishati ya kijani yahimiza maendeleo yenye sifa bora katika Mkoa wa Xizang, China

Madaraja ya matao yenye mapaa ya mbao yahifadhiwa vizuri katika Mkoa wa Fujian, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
