Mwanafunzi wa Saudi Arabia akumbatia fursa katika ushirikiano wa nishati kati ya China na Saudi Arabia

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Julai 22, 2026
Mwanafunzi wa Saudi Arabia akumbatia fursa katika ushirikiano wa nishati kati ya China na Saudi Arabia
Rimaz Dakhilallah Aljohani (katikati) akijaribu kuchomelea kwenye Tawi la Tianjin la Kiwanda cha Uzalishaji kwa Kutumia AI cha Kampuni ya Uhandisi wa Mafuta Baharini (COOEC) mjini Tianjin, kaskazini mwa China, Julai 9, 2026. (Xinhua/Sun Fanyue)

Rimaz Dakhilallah Aljohani, mwanafunzi wa shahada ya kwanza mwenye umri wa miaka 22 anayesomea uhandisi wa mafuta katika Chuo Kikuu cha King Fahd cha Petroli na Madini (KFUPM) nchini Saudi Arabia, alianza programu ya mafunzo ya miezi miwili na wanafunzi wenzake sita katika Kampuni ya Uhandisi wa Mafuta Baharini ya China (COOEC) mjini Tianjin wakati wa likizo ya majira ya joto.

Kwenye Tawi la Tianjin la Kiwanda cha Uzalishaji kwa Kutumia AI cha COOEC, amepata uzoefu wa uchomeleaji kupitia teknolojia ya VR, na amejifunza kuhusu teknolojia zilizo nyuma ya ujenzi wa kimoduli wa China na utengenezaji wa vifaa vya kuchimba mafuta na gesi baharini.

Mwaka 2022, China na Saudi Arabia zilisaini mpango wa utekelezaji kwa ajili ya ushirikiano kati ya Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja na Dira ya Saudi Arabia ya 2030. Programu hiyo ya mafunzo kati ya KFUPM na COOEC inawakilisha hatua halisi katika kutekeleza mpango huo na hutoa jukwaa kwa ajili ya mawasiliano na ushirikiano kati ya vijana.

"Kiwango cha uzalishaji kwa kutumia AI na usimamizi sanifu wa miradi hapa vimenivutia sana," Rimaz amesema. "Kwa kweli ninathamini sana fursa hii kwa mafunzo ya vitendo ya kimataifa. Imenifanya kupata maarifa ya moja kwa moja kuhusu uzoefu wa viwanda ya kuchimba mafuta baharini katika China. Ninatumai kurudisha kile nilichojifunza Saudi Arabia na kuchangia katika ushirikiano wa nishati kati ya China na Saudi Arabia."

(Wahariri wa tovuti:Liu Mengxue,Zhao Jian)

Picha