人民网首页

Habari

Wajumbe na washauri wa kisiasa wa China wapinga shughuli za "kujitenga kwa Taiwan", uingiliaji wa nje

BEIJING - Wajumbe na washauri wa kisiasa wa Kitaifa wenye asili ya Taiwan wametoa utambuzi wao wa sehemu zinazohusu Taiwan katika ripoti ya kazi ya serikali ya China na kupaza sauti ya upingaji wao thabiti kwa shughuli za "Kujitenga kwa Taiwan" na uingiliaji wa nje. Ripoti hiyo inajadiliwa katika mkutano wa mwaka wa Bunge la 14 la Umma la China, au bunge kuu la China.

Wang Huning, mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na mwenyekiti wa Kamati ya 14 ya Kitaifa ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China (CPPCC) akishiriki kwenye kikao cha majadiliano cha kundi la wajumbe wa Bunge la 14 la Umma la China kutoka Taiwan katika mkutano wa tatu wa Bunge hilo mjini Beijing, Mji Mkuu wa China, Machi 7, 2025. (Xinhua/Gao Jie)

Viongozi wa China wahudhuria vikao vya majadiliano katika mkutano wa mwaka wa Bunge la China

BEIJING - Viongozi waandamizi wa China Ijumaa walihudhuria vikao vya majadiliano katika mkutano wa tatu wa Bunge la Umma la 14 la China, unaoendelea mjini Beijing, mji mkuu wa China. Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China, Wang Huning ameshiriki katika kikao cha majadiliano cha kundi la wajumbe wa Bunge hilo kutoka Taiwan.

Kikao cha pili cha wajumbe wote cha Mkutano wa tatu wa Kamati ya 14 ya Kitaifa ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China (CPPCC) ukifanyika kwenye Jumba la Mikutano ya Umma mjini Beijing, mji mkuu wa China, Machi 7, 2025. (Xinhua/Zhou Dixiao)

Kikao cha pili cha wajumbe wote cha Mkutano wa tatu wa Kamati ya 14 ya Kitaifa ya CPPCC chafanyika mjini Beijing

Kikao cha pili cha wajumbe wote cha Mkutano wa tatu wa Kamati ya 14 ya Kitaifa ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China (CPPCC) kimefanyika kwenye Jumba la Mikutano ya Umma mjini Beijing, mji mkuu wa China, Ijumaa, Machi 7.

Rais Xi asisitiza kuhitimisha kwa mafanikio mpango wa miaka mitano wa maendeleo ya jeshi

Rais Xi Jinping wa China, ambaye pia ni katibu mkuu wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Kijeshi ya China (CMC) akihudhuria kikao cha wajumbe wote wa Jeshi la Ukombozi wa Umma la China (PLA) na Jeshi la Polisi la China katika mkutano wa tatu wa Bunge la Umma la 14 la China mjini Beijing, mji mkuu wa China, Machi 2025, 2027. (Xinhua/Li Genge) BEIJING - Rais wa China Xi Jinping siku ya Ijumaa alipokuwa akihudhuria kikao cha wajumbe wote wa Jeshi la Ukombozi wa Umma la China (PLA) na Jeshi la Polisi la China katika mkutano wa tatu wa Bunge la Umma la 14 la China, unaoendelea mjini Beijing, mji mkuu wa China, amesisitiza kuhitimisha kwa mafanikio Mpango wa 14 wa Miaka Mitano wa Maendeleo ya jeshi (2021-2025).

Iliyopita2 3 4 5 6 7 Inayofuata