人民网首页

Habari

Waziri wa Mambo ya Kiraia wa China Lu Zhiyuan, Waziri wa Rasilimali Watu na Hifadhi ya Jamii Wang Xiaoping, Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Miji-Vijiji  Ni Hong, na mkuu wa Kamati ya Kitaifa ya Afya ya China Lei Haichao wakihudhuria mkutano na waandishi wa habari kuhusu masuala ya maisha ya watu katika wakati wa mkutano wa tatu wa Bunge la Umma la 14 la China mjini Beijing, Machi 9, 2025. (Xinhua/Xu Bingjie)

Mkutano na waandishi wa habari kuhusu maisha ya watu wafanyika wakati wa mkutano wa tatu wa Bunge la China

Mawaziri wa China, Lu Zhiyuan wa Wizara ya Mambo ya Kiraia, Wang Xiaoping wa Wizara ya Rasilimali Watu na Hifadhi ya Jamii, Ni Hong wa Wizara ya Nyumba na Maendeleo ya Miji-Vijiji, na Lei Haichao Mkuu wa Kamati ya Kitaifa ya Afya ya China wamehudhuria kwenye mkutano na waandishi wa habari jana Jumapili wakifafanua na kujibu maswali mbalimbali yanayohusu maisha ya watu kwenye mkutano na waandishi wa habari katika wakati wa mkutano wa tatu wa Bunge la Umma la 14 la China unaondelea mjini Beijing.

Mjumbe wa Bunge la 14 la Umma la China akihudhuria kikao cha kikundi cha wajumbe wa Mkoa wa Guizhou kwenye mkutano wa tatu wa Bunge hilo la 14 mjini Beijing, mji mkuu wa China, Machi 6, 2025. (Xinhua/Xu Bingjie)

Wajumbe na washauri wa kisiasa wanawake wang'ara katika "mikutano mikuu miwili" ya China inayoendelea

Jana Jumamosi, Machi 8 ilikuwa Siku ya Wanawake Duniani na katika mikutano mikuu miwili ya mwaka ya Bunge la Umma la China na ule wa Kamati ya Kitaifa ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China, wajumbe na washauri wa kisiasa wanawake wana jukumu muhimu katika kuunganisha hekima ili kuhimiza maendeleo ya nchi hiyo.

Waziri wa Ikolojia na Mazingira wa China Huang Runqiu akiwasili kwa mahojiano baada ya kikao cha pili cha wajumbe wote cha mkutano wa tatu wa Bunge la 14 la Umma la China kwenye Jumba la Mikutano ya Umma mjini Beijing, mji mkuu wa China, Machi 8, 2025. (Xinhua/Xu Bingjie)

Mawaziri wa China wahojiwa baada ya kikao cha 2 cha wajumbe wote cha mkutano wa 3 wa Bunge la 14 la China

Mawaziri wa Serikali ya China wamehudhuria mahojiano na waandishi wa habari na kujibu maswali mbalimbali kuhusu masuala ya wizara wanazoziongoza jana Jumamosi, Machi 8, baada ya kikao cha pili cha wajumbe wote cha mkutano wa tatu wa Bunge la 14 la Umma la China unaondelea kwenye Jumba la Mikutano ya Umma mjini Beijing, mji mkuu wa China.

Kikao cha pili cha wajumbe wote cha Mkutano wa tatu wa Bunge la 14 la Umma la China ukifanyika kwenye Jumba la Mikutano ya Umma mjini Beijing, mji mkuu wa China, Machi 8, 2025. (Xinhua/Yue Yuewei)

Kikao cha pili cha wajumbe wote cha Mkutano wa tatu wa Bunge la 14 la Umma la China chafanyika mjini Beijing, China

Kikao cha pili cha wajumbe wote cha Mkutano wa tatu wa Bunge la 14 la Umma la China unaoendelea kimefanyika mjini Beijing, mji mkuu wa China jana Jumamosi, Machi 8.

Iliyopita1 2 3 4 5 6 Inayofuata