LUSAKA - Mirriam Chola, mwanafunzi katika Jimbo la Copperbelt la Zambia, kwa muda mrefu alikuwa akiota kuhudhuria shule ambayo anaweza kufika kwa kutembea kwa miguu kutoka nyumbani kwake huko Kalulushi, mji wa pembezoni karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. "Nilikuwa nikisoma katika shule ya Katoliki ambapo nilikuwa na changamoto ya kuwa pamoja na familia yangu, na nilikuwa nikiwakumbuka sana," Chola amekumbushia.
Tokea Mei 1, China ilianza kutekeleza sera ya ushuru-sifuri kwa bidhaa kutoka nchi 53 za Afrika ambazo inadumisha uhusiano wa kidiplomasia nazo. Kwa mujibu wa Kampuni ya Uendeshaji wa Reli ya Africa Star, Reli ya SGR ya Kenya iliendesha treni za mizigo jumla ya 3,931 katika nusu ya kwanza ya mwaka 2026, ikisafirisha tani milioni 4.
ADDIS ABABA - Maafisa kutoka China na Umoja wa Afrika (AU) wamesisitiza umuhimu wa Maonyesho ya Uagizaji na Uuzaji Nje Bidhaa ya China, ambayo pia yanajulikana kwa jina la Maonyesho ya Canton, katika kuunganisha biashara za Afrika na wanunuzi, wawekezaji, washirika wa teknolojia, na fursa mpya za kibiashara duniani. Kauli hiyo imetolewa kwenye mkutano uliofanyika Jumanne wiki hii katika makao makuu ya AU mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, ili kutangaza Maonyesho ya 140 ya Canton.
PRETORIA, Afrika Kusini - Kampuni ya kuunda magari ya Chery ya China imezindua rasmi kiwanda chake cha kuzalisha magari siku ya Ijumaa huko Rosslyn, kaskazini mwa mji mkuu wa utawala wa Afrika Kusini, Pretoria, ikiashiria mabadiliko yake ya kuwa mzalishaji magari wa nchini humo na kuzidisha dhamira yake ya muda mrefu kwa soko la Afrika Kusini. Akihutubia hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho, Mwenyekiti wa Chery Yin Tongyue amesema uwekezaji huo unaonyesha dhamira ya muda mrefu ya kampuni hiyo kwa Afrika Kusini.