Jumamosi, Mei 23 Tamasha la Utamaduni la Siku ya Afrika kwa Waafrika wanaoishi China lilifanyika mjini Beijing, mji mkuu wa China likivutia watu wengi kuja kujionea utajiri wa utamaduni wa Afrika na mambo mbalimbali yanayowakilisha ushirikiano na ukaribu wa muda mrefu wa kati ya China na Afrika. Katika tamasha hilo, moja ya vivutio vikubwa ilikuwa mitindo ya mavazi ya kijadi kutoka tamaduni mbalimbali za Afrika.
Tamasha la wazi la Siku ya Afrika mwaka 2026 likifanyika mjini Beijing, China, Mei 23, 2026. (Picha na People’s Daily Online) Tamasha la wazi la Siku ya Afrika mwaka 2026 kwa Waafrika wanaoishi China limefanyika mjini Beijing, China juzi Jumamosi likiwaleta pamoja wanadiplomasia wanaoziwakilisha nchi mbalimbali duniani hususani za Afrika, maofisa wa serikali ya China, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa nchini China na watu wa pande mbili za China na Afrika kusherehekea utajiri wa kitamaduni wa Afrika.
Kuanzia tarehe Mosi, Mei, China imeanza kutekeleza sera ya kutotoza ushuru kwa nchi zote 53 za Afrika zenye uhusiano wa kidiplomasia nayo. Hatua hiyo ya China imechukuliwa kuwa hatua muhimu kwa kuhimiza ufunguaji mlango na ushirikiano kati ya nchi za Dunia ya Kusini, wakati hali ya kujilinda na kuparaganyika kiuchumi inazidi kuonekana duniani kote.
Maofisa wa Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun wakifanya ukaguzi wa maparachichi freshi kutoka Kenya baada ya sera ya ushuru-sifuri kwa nchi 53 zenye uhusiano wa kidiplomasia na China kuanza kutekelezwa, Mei 1, 2026. (Picha kwa hisani ya Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun) Tufaha freshi kutoka Afrika Kusini, machungwa freshi ya Misri, maparachichi freshi ya Kenya.