人民网首页

Picha

Wanafunzi wakihudhuria darasa katika Shule ya Sekondari ya Minsenga iliyojengwa na Kampuni ya Sino-Metals Leach Tawi la Zambia, Kalulushi, Jimbo la Copperbelt, Zambia, Julai 14, 2026. (Picha na Martin Mbangweta/Xinhua)

Kampuni za China zapanua njia ya kufikia elimu kwa watoto wa vijijini nchini Zambia

LUSAKA - Mirriam Chola, mwanafunzi katika Jimbo la Copperbelt la Zambia, kwa muda mrefu alikuwa akiota kuhudhuria shule ambayo anaweza kufika kwa kutembea kwa miguu kutoka nyumbani kwake huko Kalulushi, mji wa pembezoni karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. "Nilikuwa nikisoma katika shule ya Katoliki ambapo nilikuwa na changamoto ya kuwa pamoja na familia yangu, na nilikuwa nikiwakumbuka sana," Chola amekumbushia.

Picha hii iliyopigwa Julai 10, 2026 ikionyesha treni ya mizigo kwenye Reli ya SGR ya Mombasa-Nairobi ikiingia katika Stesheni ya Reli ya Port Reitz, Mombasa, Kenya. (Xinhua/Xie Jianfei)

Reli ya SGR ya Kenya yashuhudia ongezeko la mizigo baada ya kuanza kwa sera ya ushuru-sifuri ya China

Tokea Mei 1, China ilianza kutekeleza sera ya ushuru-sifuri kwa bidhaa kutoka nchi 53 za Afrika ambazo inadumisha uhusiano wa kidiplomasia nazo. Kwa mujibu wa Kampuni ya Uendeshaji wa Reli ya Africa Star, Reli ya SGR ya Kenya iliendesha treni za mizigo jumla ya 3,931 katika nusu ya kwanza ya mwaka 2026, ikisafirisha tani milioni 4.

Jiang Feng, mkuu wa Ujumbe wa China katika Umoja wa Afrika (AU), akitoa hotuba kwenye mkutano wa kutangaza Maonyesho ya 140 ya Canton katika makao makuu ya AU, Addis Ababa, Ethiopia, Julai 7, 2026. (Xinhua/Geng Xinning)

Maonyesho ya Canton yatangazwa katika AU ili kuunganisha biashara za Afrika na wanunuzi duniani

ADDIS ABABA - Maafisa kutoka China na Umoja wa Afrika (AU) wamesisitiza umuhimu wa Maonyesho ya Uagizaji na Uuzaji Nje Bidhaa ya China, ambayo pia yanajulikana kwa jina la Maonyesho ya Canton, katika kuunganisha biashara za Afrika na wanunuzi, wawekezaji, washirika wa teknolojia, na fursa mpya za kibiashara duniani. Kauli hiyo imetolewa kwenye mkutano uliofanyika Jumanne wiki hii katika makao makuu ya AU mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, ili kutangaza Maonyesho ya 140 ya Canton.

Makamu Rais wa Afrika Kusini Paul Mashatile akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuzalisha magari cha Chery, Pretoria, Afrika Kusini, Julai 3, 2026. (Xinhua/Chen Wei)

Kampuni ya kuunda magari ya Chery ya China yafungua kiwanda cha kwanza Afrika Kusini, yalenga soko pana la Afrika

PRETORIA, Afrika Kusini - Kampuni ya kuunda magari ya Chery ya China imezindua rasmi kiwanda chake cha kuzalisha magari siku ya Ijumaa huko Rosslyn, kaskazini mwa mji mkuu wa utawala wa Afrika Kusini, Pretoria, ikiashiria mabadiliko yake ya kuwa mzalishaji magari wa nchini humo na kuzidisha dhamira yake ya muda mrefu kwa soko la Afrika Kusini. Akihutubia hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho, Mwenyekiti wa Chery Yin Tongyue amesema uwekezaji huo unaonyesha dhamira ya muda mrefu ya kampuni hiyo kwa Afrika Kusini.

上一页1 2 3 4 5 6 下一页