Maji machafu yaliyochafuliwa kwa mionzi ya nyuklia ya Japani yachochea hasira (2)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Septemba 04, 2023

Watu wakishiriki kwenye maandamano huko Suva, Fiji, tarehe 25 Agosti, wakipinga Japan kutiririsha maji yenye sumu ya nyuklia hivi karibuni kwenye Bahari ya Pasifiki. (SANG QINLONG/XINHUA)

Watu wakishiriki kwenye maandamano huko Suva, Fiji, tarehe 25 Agosti, wakipinga Japan kutiririsha maji yenye sumu ya nyuklia hivi karibuni kwenye Bahari ya Pasifiki. (SANG QINLONG/XINHUA)

Pamoja na upinzani mwingi ndani na nje ya nchi, Japan mnamo Agosti 24 ilianza kutiririsha maji machafu kutoka kinu cha nyuklia cha Fukushima Daiichi kilichoharibika vibaya.

"Hii ni hatua ya maafa na mbaya sana ya Japan," amesema Lusia Lagilevo, mmoja wa waandamanaji kutoka Jukwaa la Kikatiba la NGO. "Ni kutoheshimu haki zetu kama binadamu."

"Ingawa tunatoka nchi ndogo za visiwa, bado tunastahili kuheshimiwa kwa haki zetu, hadhi yetu, na uhuru wetu," Lagilevo ameliambia Shirika la Habari la China, Xinhua.

Maelfu ya wavuvi, wanaharakati, na wanasiasa wa Korea Kusini wamefanya maandamano katikati ya Seoul siku ya Jumamosi, wakilaani Japan kutiririsha maji machafu yenye sumu ya nyuklia.

(Wahariri wa tovuti:Shixi,Zhao Jian)

Picha