Mji wa Yangzhou wa China wahimiza utalii wa kitamaduni kwa kutumia Mfereji Mkuu wa China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Mei 27, 2025
Mji wa Yangzhou wa China wahimiza utalii wa kitamaduni kwa kutumia Mfereji Mkuu wa China
Msanii anacheza densi kwenye Mfereji Mkuu wa China mjini Yangzhou, Mkoa wa Jiangsu, mashariki mwa China, Mei 19, 2025. (Xinhua/Chen Shuo)

Ukiwa ni moja ya miji maarufu ya kale ya China, mji wa Yangzhou katika Mkoa wa Jiangsu, mashariki mwa China una historia ya miaka zaidi ya 2,500. Unatumia vya kutosha rasilimali za utalii wa kitamaduni za Mfereji Mkuu wa China, kufuatilia na kuendeleza mandhari na miundo mipya, na kuanzisha miradi ya utalii wa kitamaduni kwa utalii wa matembezi ya usiku ya mfereji huo ili kuingiza uhai mpya katika mji huo wa kale.

Mfereji Mkuu wa China unaunganisha Beijing na Hangzhou katika Mkoa wa Zhejiang mashariki mwa China, ukiwa ulitumika kama ateri muhimu ya usafirishaji katika China ya kale. Mfereji huo wenye urefu wa kilomita zaidi ya 1,000 ulitangazwa kuwa eneo la Urithi wa Dunia mwaka 2014.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha