Ethiopia yaokoa dola bilioni 3.1 kupitia mbadala wa uagizaji bidhaa ndani ya miezi 9

(CRI Online) Mei 30, 2025

Ethiopia imeokoa dola za Kimarekani zaidi ya bilioni 3.1 kupitia kubadilisha bidhaa zinazoagizwa kutoka nje kwa mbadala wa zile zinazozalishwa nchini katika muda wa miezi tisa ya kwanza ya mwaka huu wa fedha, ulioanza Julai 8, 2024.

Kwa mujibu wa Waziri wa Viwanda wa Ethiopia Tarekegn Bululta, soko la nchi hiyo limeongezeka kutoka asilimia 30 hadi asilimia 44 katika miaka michache iliyopita, kutokana na maboresho ya hivi karibuni katika sekta ya viwanda, ikiokoa fedha za kigeni zinazohitajika sana ambazo zingetumika kuagiza bidhaa kutoka nje.

Akisisitiza umuhimu wa kimkakati wa sekta hiyo katika kufikia ukuaji endelevu, shindani na thabiti wa uchumi, amesema maendeleo hayo ya hivi karibuni ni matokeo ya juhudi ratibiwa zinazolenga kushughulikia masuala ya kimfumo.

Aidha, Bululta ametilia mkazo maboresho makubwa katika sekta ya utengenezaji kama vile nguo, chuma, chakula na vinywaji.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha