

Lugha Nyingine
Kusherehekea Sikukuu ya Mashua ya Dragon mahali pa chimbuko lake la kihistoria
Kwenye pande za Mto Miluo mkoani Hunan, katikati mwa China, mila na desturi za jadi kama vile mashindano ya mbio za Mashua ya dragon, kula zongzi (chakula cha wali wa kunata) na kutundika kifurushi cha majani ya mugwort zimekuwa zikirithishwa kwa maelfu ya miaka, zikiunda utambulisho wa kipekee wa kiutamaduni.
Hadithi inasema kwamba miaka zaidi ya 2,300 iliyopita, mshairi Qu Yuan wa China alijiua katika Mto Miluo, akiacha urithi wa kudumu wa uzalendo na ushairi. Tangu wakati huo, Miluo imekuwa ikisherehekewa kama chimbuko la Sikukuu ya Mashua ya Dragon, nyumbani kwa a Mashua ya dragon, na chimbuko la mashairi ya jadi ya China.
Kwa zaidi ya miaka 2,000 iliyopita, jadi za Sikukuu ya Mashua ya Dragon, pia ikijulikana kwa jina la Sikukuu ya Duanwu, zimekuwa zikihifadhiwa na kurithishwa vizazi hadi vizazi katika eneo hilo lenye rasilimali nyingi za kiutamaduni.
Ungana na mwandishi wa habari wa People’s Daily Online Michael Kurtagh kando ya Mto Miluo anapofurahia msisimko wa mashindano ya mbio za Mashua ya dragon kwa kushiriki mwenyewe na kujichangamisha mwenyewe katika uzuri wa kudumu wa utamaduni wa kijadi wa China.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma