

Lugha Nyingine
OECD lapunguza makadirio ya ongezeko la uchumi wa dunia kwa mwaka huu na ujao
(CRI Online) Juni 04, 2025
Shirika la Ushirikiano na Maendeleo ya Kiuchumi (OECD) limetoa ripoti yake mpya ya mtazamo wa uchumi duniani jana Jumanne, likikadiria kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi duniani itakuwa 2.9% mwaka 2025 na 2.9% mwaka 2026, ikiwa ni punguzo la asilimia 0.2 na asilimia 0.1 mtawalia kutoka kwenye makadirio ya awali ya mwezi Machi mwaka huu.
Ripoti hiyo imesema, katika miezi kadhaa iliyopita, vizuizi vya biashara pamoja na hali ya kutokuwa na uhakika kwa sera za kiuchumi na kibiashara vimeongezeka kwa kiasi kikubwa, vikiathiri vibaya biashara na imani za wateja, na pia kuzuia biashara na uwekezaji.
Mazingira hayo magumu ya kiuchumi na kibiashara duniani yamelifanya OECD kupunguza tena makadirio yake ya ukuaji wa uchumi duniani kwa mwaka huu na ujao.
(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma