Umoja wa Afrika waeleza wasiwasi kuhusu vizuizi vya usafiri vilivyowekwa na Marekani

(CRI Online) Juni 06, 2025

Kamisheni ya Umoja wa Afrika imeeleza wasiwasi kuhusu vizuizi vya usafiri vilivyowekwa na Marekani dhidi ya raia wa nchi mbalimbali.

Katika taarifa yake iliyotolewa jana Alhamisi, Kamisheni hiyo imesema, ingawa kila nchi ina haki ya kulinda mipaka yake na kuwalinda raia wake, lakini inatumai kuwa Marekani itatumia haki hiyo kwa usawa na kwa msingi wa uhalisia wa mambo.

Taarifa hiyo pia imesema, vizuizi hivyo vinawezekana kuathiri vibaya nchi mbalimbali za Afrika na Marekani katika mabadilishano ya utamaduni na jamii, ushirikiano wa elimu na biashara, na uhusiano wa kibalozi, na kutoa wito kwa serikali ya Marekani kuchukua hatua na kufanya mazungumzo na nchi husika.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha