Maonyesho ya 3 ya Kimataifa ya Uchukuzi wa Meli ya Tianjin, China yaanza (3)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 13, 2025
Maonyesho ya 3 ya Kimataifa ya Uchukuzi wa Meli ya Tianjin, China yaanza
Watu wakitazama mifano ya meli kwenye Maonyesho ya 3 ya Kimataifa ya Uchukuzi wa Meli ya Tianjin mjini Tianjin, kaskazini mwa China, Juni 12, 2025. (Xinhua/Li Ran)

Maonyesho ya 3 ya Kimataifa ya Uchukuzi wa Meli ya Tianjin yameanza mjini Tianjin, kaskazini mwa China jana Alhamisi. Yakifanyika chini ya kaulimbiu ya "Kusafirisha kwa Meli kwenda Duniani na kuelekea Siku za Baadaye", maonyesho hayo ya siku tatu yanafuatilia mienendo na fursa zinazoibuka katika mnyororo wa uchukuzi wa meli duniani.

Kampuni zaidi ya 440 zinashiriki kwenye maonyesho hayo yanayochukua eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 50,000 na yakijumuisha maeneo 9 ya maonyesho, kama vile bandari za kimataifa, uchukuzi wa meli wa kijani na kisasa, mnyororo wa viwanda vya uchukuzi wa meli na mambo mengine.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Renato Lu)

Picha