Habari katika picha: Shamba kama kiwanda linalotumia teknolojia za kisasa mjini Kuqa, Xinjiang nchini China (4)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Agosti 15, 2025
Habari katika picha: Shamba kama kiwanda linalotumia teknolojia za kisasa mjini Kuqa, Xinjiang nchini China
Mfanyakazi akivuna mboga kwenye shamba la kisasa linalofanana na kiwanda mjini Kuqa, eneo la Aksu Mkoani Xinjiang, China Agosti 13, 2025. (Xinhua/Liu Jiaqi)

Shamba la kisasa linalofanana na kiwanda katika mji wa Kuqa, linaonekana kuwa ni mradi mkuu wa mpango wa msaada unaogharamiwa na mji wa Ningbo ulioko Mkoani Zhejiang mashariki mwa China. Shamba hilo mfano wa kiwanda linaweza kuzalisha mazao ya kilimo kwa mwaka mzima kupitia udhibiti wa halijoto, unyevu, mwanga na virutubisho.

Ikiwa ni hatua muhimu ya ushirikiano kati ya mji wa Ningbo na Kuqa, mradi huo umetumia teknolojia na vifaa vya kilimo bila kutumia udongo vinavyotolewa na makampuni ya Ningbo kuzalisha mazao bora ya kilimo.

(Wahariri wa tovuti:Shixi,Zhao Jian)

Picha