

Lugha Nyingine
Wang Yi akutana na mjumbe maalum wa Rais wa Korea Kusini Park Byung-seok
Waziri wa Mambo ya Nje Wang Yi jana alikutana na Mjumbe Maalum wa Rais wa Korea Kusini Park Byung-seok mjini Beijing.
Wang Yi amesema kuwa baada ya serikali mpya ya Korea Kusini kuchukua madaraka, rais Xi Jinping na mwenzake Lee Jae-myung wamefanya mazungumzo kwa njia ya simu na kufikia makubaliano muhimu ya kuinua ushirikiano wa kimkakati kati ya China na Korea Kusini hadi ngazi ya juu na kuelekeza maendeleo ya baadaye ya uhusiano wa nchi hizo mbili. Pande zote mbili zinapaswa kuzingatia matarajio ya awali ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia, kubaki na nia ya urafiki, kupanua maslahi ya pamoja, kuboresha hisia za umma, na kushughulikia ipasavyo masuala nyeti.
Park Byung-seok alimwomba Wang Yi kuwasilisha barua inayotoka kwa Rais Lee Jae-myung kwa Rais Xi Jinping, akieleza nia ya serikali mpya ya Korea Kusini kurejesha uhusiano wa ushirikiano wa kimkakati kati ya Korea Kusini na China. Korea Kusini siku zote inaheshimu Kanuni ya kuwepo kwa China Moja na iko tayari kuendeleza uhusiano wa usawa na mataifa makubwa kama vile China.
Uwekaji wa nguzo za chuma kwenye Daraja la Mto Hanjiang la reli ya kasi ya Xi'an-Shiyan wakamilika
Michezo ya Dunia ya Chengdu | Sherehe ya Kufungwa kwa Michezo ya 12 ya Dunia yafanyika
Reli ya kasi China iliyoko kaskazini zaidi mwa China yafikisha miaka 10 tangu ilipoanzishwa
Mandhari ya Arxan yenye vivutio vingi vya utalii, Kaskazini mwa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma