

Lugha Nyingine
Iran yakataa kithabiti madai ya Marekani ya kutii masharti yake
Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei amesema, Marekani inajaribu kuilazimisha Iran kutii masharti yake kwa kuiwekea vizuizi.
Katika hotuba yake aliyoitoa jana jumapili mjini Tehran, Bw. Khamenei amesema, wale wanaounga mkono Iran kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na Marekani ili kutatua suala hilo hawana busara, na amesisitiza kuwa Iran itapinga kithabiti madai ya Marekani.
Pia amesema, Marekani inatarajia Iran kuitii, jambo linalowakasirisha sana watu wa Iran, ambao wako tayari kupambana kwa nguvu zake zote dhidi ya wale wanaounga mkono kitendo hicho cha Marekani.
Bw. Khamenei pia ameonya wapinzani wanaojaribu kutimiza malengo yao kwa kuzusha migawanyiko ndani ya Iran, na kutoa wito wa kuongeza juhudi katika kudumisha na kuimarisha umoja wa sasa.
Uwekaji wa nguzo za chuma kwenye Daraja la Mto Hanjiang la reli ya kasi ya Xi'an-Shiyan wakamilika
Michezo ya Dunia ya Chengdu | Sherehe ya Kufungwa kwa Michezo ya 12 ya Dunia yafanyika
Reli ya kasi China iliyoko kaskazini zaidi mwa China yafikisha miaka 10 tangu ilipoanzishwa
Mandhari ya Arxan yenye vivutio vingi vya utalii, Kaskazini mwa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma