

Lugha Nyingine
Watu 20 wauawa katika mashambulizi ya jeshi la Israel kwenye hospitali ya Gaza
Watu zaidi ya 20 wakiwemo waandishi wa habari watano wameuawa jana baada ya jeshi la Israel kushambulia mara mbili hospitali ya Nasser huko Khan Yunis, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
Chanzo cha usalama cha Ukanda wa Gaza kimeliambia Shirika la habari la China Xinhua kwamba, ndege za kivita za Israel zilishambulia kwanza hospitali ya Nasser na kisha kuwashambulia wafanyakazi wa afya waliokuwa wakifanya uokoaji.
Idara ya Afya ya Ukanda wa Gaza imetoa taarifa ikisema, miongoni mwa watu waliokufa ni pamoja na wafanyakazi wa matibabu, wagonjwa, waandishi wa habari, na wafanyakazi wa ulinzi wa raia, na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Uwekaji wa nguzo za chuma kwenye Daraja la Mto Hanjiang la reli ya kasi ya Xi'an-Shiyan wakamilika
Michezo ya Dunia ya Chengdu | Sherehe ya Kufungwa kwa Michezo ya 12 ya Dunia yafanyika
Reli ya kasi China iliyoko kaskazini zaidi mwa China yafikisha miaka 10 tangu ilipoanzishwa
Mandhari ya Arxan yenye vivutio vingi vya utalii, Kaskazini mwa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma