Mabadiliko ya Kijiji cha Yuhu Kusini-Magharibi mwa China kutoka umaskini hadi ustawi (2)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Januari 20, 2026
Mabadiliko ya Kijiji cha Yuhu Kusini-Magharibi mwa China kutoka umaskini hadi ustawi
Picha iliyopigwa kutoka Kijiji cha Yuhu ikionyesha mandhari ya Mlima wa Theluji wa Yulong, katika Mji wa Lijiang, Mkoa wa Yunnan, kusini magharibi mwa China, Januari 17, 2026. (Xinhua/Wang Guansen)

Kijiji cha Yuhu, kilichopo katika Mji mdogo wa Baisha wa Wilaya Inayojiendesha ya Kabila la Wanaxi ya Yulong katika Mji wa Lijiang mkoani Yunnan, China ni moja ya makazi ya mapema zaidi ya watu wa kabila la Wanaxi. Kijiji hicho kilikuwa miongoni mwa vijiji maskini zaidi katika Mji wa Lijiang kwa sababu ya udongo wake duni na njia zisizotosheleza za usafiri.

Katika miaka ya hivi karibuni, kijiji hicho cha Yuhu kimeendeleza njia ya kipekee inayowianisha ukuaji wa uchumi na ulinzi wa mazingira. Kwa kutumia ipasavyo urithi wake wa kiutamaduni wa Kabila la Wanaxi uliohifadhiwa vizuri na mandhari ya kipekee ya mazingira ya asili, kijiji hicho kimevutia watalii kutoka sehemu mbalimbali duniani. Wakati huo huo, kimeendelea kuboresha miundombinu na huduma za umma, na kuvutia idadi inayoongezeka ya wakazi wenyeji kurudi nyumbani kwa biashara.

Katika kipindi cha Mwaka 2025, Kijiji cha Yuhu kilikaribisha safari takribani milioni 1.2 za watalii, kikizalisha mapato ya yuan milioni 75 (dola za Marekani milioni 10.8) -- huku wastani wa mapato ya kila mtu kwa wenyeji ukiongezeka kutoka yuan 13,000 (dola za Marekani 1,865) katika mwaka 2019 hadi yuan takriban 35,000 (dola za Marekani 5,022).

(Wahariri wa tovuti:Liu Mengxue,Zhao Jian)

Picha