人民网首页

Habari

Rais wa China ahutubia ufunguzi wa mkutano wa 139 wa wajumbe wote wa Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa

(Picha inatoka CRI.) Rais Xi Jinping wa China leo ametoa hotuba kwa njia ya video katika ufunguzi wa mkutano wa 139 wa wajumbe wote wa Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa.

Kamati ya Olimpiki ya Beijing 2022 yasema China haidanganyi kamwe majibu ya vipimo vya UVIKO-19

Picha iliyopigwa Januari 10, 2022 ikionesha vifaa vya kudhibiti janga la UVIKO-19 katika Kituo Kikuu cha Vyombo vya Habari kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki na Michezo ya Olimpiki ya Walemavu ya Majira ya Baridi ya Mwaka 2022 huko Beijing. (Xinhua/Xu Zijian) BEIJING - Huang Chun, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Kuzuia na Kudhibiti Janga la Virusi vya Korona ya Kamati ya Maandalizi ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing 2022 amesema kwamba, haina haja ya kudanganya matokeo ya vipimo vya UVIKO-19, na China kamwe haitafanya hivyo.

Rais Xi kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing 2022

Mwenge wa Olimpiki kwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing 2022 ukioneshwa kwenye Mnara wa Olimpiki huko Beijing, Mji Mkuu wa China, Oktoba 20, 2021. (Xinhua/Wang Yong) BEIJING - Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China, Hua Chunying ametangaza Ijumaa ya wiki hii kwamba, kuanzia Februari 4 hadi 6, Rais Xi Jinping wa China atahudhuria sherehe za ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing 2022, na kufanya hafla ya kuwakaribisha wakuu wa nchi mbalimbali duniani, wakuu wa serikali, wajumbe wa familia za kifalme na wakuu wa mashirika ya kimataifa watakaohudhuria sherehe hiyo, na kufanya shughuli mbalimbali husika za uhusiano wa pande mbili.

Mwandishi wa habari akipiga picha za eneo la mchanganyiko la Kijiji cha Olimpiki kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing 2022 huko Zhangjiakou, Mkoa wa Hebei Kaskazini mwa China, Januari 27, 2022. Vijiji vya Olimpiki kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing 2022 kile cha Yanqing, Mjini Beijing, Mji Mkuu wa China na kile cha Zhangjiakou mkoani Hebei, Kaskazini mwa China vimefungua rasmi milango yao kwa wanamichezo na maafisa wa timu kwa Michezo hiyo siku ya Alhamisi ya wiki hii. (Xinhua/Xiong Qi)

Vijiji vya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing 2022 vyafunguliwa rasmi

BEIJING - Vijiji vya Olimpiki kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing 2022 cha eneo la Yanqing, mjini Beijing na Zhangjiakou, Mkoa wa Hebei vilifungua milango yao kwa wanamichezo na maafisa wa timu kwa ajili ya Michezo hiyo siku ya Alhamisi ya wiki hii. Zhang Guannan, mfanyakazi wa timu ya uendeshaji wa Kijiji cha Olimpiki cha Beijing, amesema kijiji hicho kitawapokea wanamichezo 1,000 na maafisa wa timu kutoka nchi na kanda 44.

Iliyopita11 12 13 14 15 16 Inayofuata