人民网首页

Habari

Wakati wa usiku wa Januari 27, washiriki na watu wa kujitolea wa maandalizi ya hafla ya kutunuku medali ya Michezo ya Olimpiki walifanya mazoezi ya mchakato wa utoaji medali.(Picha/Xinhua)

Washiriki Kwenye Maandalizi Wafanya Mazoezi ya hafla ya kutunuku medali ya Michezo ya Olimpiki

Kwa kuwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing imekaribia, majaribio ya mwisho ya zana na vifaa na mazoezi ya mwisho ya mchakato mzima wa michezo hiyo yanafanyika kwenye uwanja wa utoaji wa medali wa Beijing, uwanja huo uko karibu na Uwanja wa Michezo wa Taifa “Kiota cha Ndege”.

Afisa Mwandamizi wa CPC atoa wito kwa vyombo vya habari vya kimataifa kutoa habari za Michezo ya Olimpiki ya Beijing 2022

BEIJING -- Afisa Mwandamizi wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), Huang Kunming Jumatano ya wiki hii ameelezea matumaini yake kwamba marafiki kutoka vyombo vya habari vya kimataifa watashiriki kutoa habari chanya za Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing na kuonesha Michezo hiyo ya Olimpiki ya "kuvutia, ajabu na bora". Huang Kunming, Mjumbe wa Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya CPC na Mkuu wa Idara ya Uenezi ya Kamati Kuu ya CPC, ameyasema hayo alipokuwa akihutubia kwenye ufunguzi wa Kongamano la kwanza la Kituo kikuu cha Radio na Televisheni cha China (CMG).

Wizara ya Mambo ya Nje ya China yasifu sana uungaji mkono wa Rais Putin wa Russia kwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Zhao Lijian alisema Januari 26 kuwa upande wa China unasifu sana uungaji mkono wa Rais Vladimir Putin wa Russia kwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing. Ameeleza matumaini yake kuwa wanamichezo wa nchi mbalimbali wakiwemo pamoja na wanamichezo wa Russia watapata mafanikio bora na kung'ara kwenye uwanja wa mashindano ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing.

Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing kuimarisha mawasiliano ya kirafiki kati ya vijana duniani

Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon amesema anaamini kuwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing itapata mafanikio makubwa na kuimarisha mawasiliano ya kirafiki kati ya vijana wa nchi mbalimbali zikiwemo Korea Kusini na China.

Iliyopita12 13 14 15 16 17 Inayofuata