(Picha/Xinhua) Mazungumzo kati ya vijana wa China na Afrika yamefanyika Alhamis katika mji wa Pretoria, Afrika Kusini, na kukutanisha wawakilishi wa vijana waliobadilishana maoni kuhusu uhusiano wa pande mbili, ushirikiano wa Kusini na Kusini, maendeleo ya vijana na ushirikiano wa pande nyingi. Chini ya kaulimbiu "Ushirikiano wa Kusini na Kusini katika Dunia ya Pande Nyingi," washiriki walisema ushiriki wa vijana una umuhimu mkubwa katika kuunda ushirikiano duniani.
Kuanzia tarehe Mosi, Mei, China imeanza kutekeleza sera ya kutotoza ushuru kwa nchi zote 53 za Afrika zenye uhusiano wa kidiplomasia nayo. Hatua hiyo ya China imechukuliwa kuwa hatua muhimu kwa kuhimiza ufunguaji mlango na ushirikiano kati ya nchi za Dunia ya Kusini, wakati hali ya kujilinda na kuparaganyika kiuchumi inazidi kuonekana duniani kote.
Maofisa wa Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun wakifanya ukaguzi wa maparachichi freshi kutoka Kenya baada ya sera ya ushuru-sifuri kwa nchi 53 zenye uhusiano wa kidiplomasia na China kuanza kutekelezwa, Mei 1, 2026. (Picha kwa hisani ya Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun) Tufaha freshi kutoka Afrika Kusini, machungwa freshi ya Misri, maparachichi freshi ya Kenya.
ZANZIBAR, Tanzania - Kwa miaka mitano, Selemani Juma Selemani Mtanzania mwenye umri wa miaka 24 amekuwa akiishi na hali ya maumivu, homa, na kukosa utulivu kwa kudumu kutokana na hali ngumu ya mfumo wa mkojo ambayo imekuwa ikimsumbua maisha yake ya kila siku. Akiwa ni mfanyakazi wa hoteli katika Kisiwa cha Unguja, Zanzibar, Tanzania, Selemani alikuwa akihangaika kudumisha utaratibu wa kawaida.