人民网首页

Habari

Mazungumzo ya vijana wa China na Afrika yafanyika nchini Afrika Kusini

(Picha/Xinhua) Mazungumzo kati ya vijana wa China na Afrika yamefanyika Alhamis katika mji wa Pretoria, Afrika Kusini, na kukutanisha wawakilishi wa vijana waliobadilishana maoni kuhusu uhusiano wa pande mbili, ushirikiano wa Kusini na Kusini, maendeleo ya vijana na ushirikiano wa pande nyingi. Chini ya kaulimbiu "Ushirikiano wa Kusini na Kusini katika Dunia ya Pande Nyingi," washiriki walisema ushiriki wa vijana una umuhimu mkubwa katika kuunda ushirikiano duniani.

Picha hii iliyopigwa tarehe 23, Machi, 2026 ikionesha treni ya mizigo ikiegesha kwenye Stesheni ya Nairobi ya Reli ya Mombasa-Nairobi. (Picha na Nelson Asienwa/Xinhua)

Sera ya kutotoza ushuru yahimiza mchakato wa maendeleo ya mambo ya kisasa ya China na Afrika

Kuanzia tarehe Mosi, Mei, China imeanza kutekeleza sera ya kutotoza ushuru kwa nchi zote 53 za Afrika zenye uhusiano wa kidiplomasia nayo. Hatua hiyo ya China imechukuliwa kuwa hatua muhimu kwa kuhimiza ufunguaji mlango na ushirikiano kati ya nchi za Dunia ya Kusini, wakati hali ya kujilinda na kuparaganyika kiuchumi inazidi kuonekana duniani kote.

Sera ya Ushuru-Sifuri Yasaidia Bidhaa Bora za Afrika Kukumbatia Soko Kubwa la China

Maofisa wa Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun wakifanya ukaguzi wa maparachichi freshi kutoka Kenya baada ya sera ya ushuru-sifuri kwa nchi 53 zenye uhusiano wa kidiplomasia na China kuanza kutekelezwa, Mei 1, 2026. (Picha kwa hisani ya Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun) Tufaha freshi kutoka Afrika Kusini, machungwa freshi ya Misri, maparachichi freshi ya Kenya.

Daktari mchina bingwa wa mfumo wa mkojo Wang Kunpeng (kulia) na mhudumu wa afya mwenyeji (kushoto) wakipiga picha na mgonjwa Selemani Juma Selemani baada ya upasuaji katika Hospitali ya Lumumba, Zanzibar, Tanzania, Januari 26, 2026. (Kundi la 35 la Timu ya madaktari Wachina visiwani Zanzibar/kupitia Xinhua)

Upasuaji wa kuokoa maisha Zanzibar waakisi ushirikiano unaokua wa afya kati ya China na Tanzania

ZANZIBAR, Tanzania - Kwa miaka mitano, Selemani Juma Selemani Mtanzania mwenye umri wa miaka 24 amekuwa akiishi na hali ya maumivu, homa, na kukosa utulivu kwa kudumu kutokana na hali ngumu ya mfumo wa mkojo ambayo imekuwa ikimsumbua maisha yake ya kila siku. Akiwa ni mfanyakazi wa hoteli katika Kisiwa cha Unguja, Zanzibar, Tanzania, Selemani alikuwa akihangaika kudumisha utaratibu wa kawaida.

1 2 3 4 5 6 Inayofuata