人民网首页

Habari

Kundi la Mabalozi wa Afrika nchini China waandaa Mapokezi ya Siku ya Afrika Kuadhimisha Miaka 63 ya AU

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China Miao Deyu akihudhuria na kutoa hotuba kwenye hafla iliyoandaliwa na Kundi la Mabalozi wa Afrika nchini China kusherehekea "Siku ya Afrika" mjini Beijing, Mei 25, 2026. (CMFA/People’s Daily Online) Kundi la Mabalozi wa Afrika nchini China (GAAC) limeandaa hafla ya mapokezi ya kidiplomasia ya ngazi ya juu jana Jumatatu jioni mjini Beijing kuadhimisha Siku ya Afrika 2026, ikiwakutanisha Wakuu wa Balozi na wanadiplomasia wa Afrika, mabalozi kutoka makundi mengine ya kikanda, maofisa waandamizi wa Serikali ya China, mawaziri wa Afrika walioko ziarani China, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, wajumbe wa diaspora wa Afrika, viongozi wa kibiashara, wasomi, na marafiki wa muda mrefu wa Afrika nchini China.

Shindano la umahiri wa lugha ya Kichina lafanyika Rwanda

Nkurunziza Tharcisse, mshindi wa fainali ya Rwanda ya Mashindano ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya "Daraja la Lugha ya Kichina" ya mwaka 2026 kwa Wanafunzi wa Vyuo, akipiga picha na Gao Wenqi, Balozi wa China nchini Rwanda, mjini Kigali, Rwanda, Mei 24, 2026. (Xinhua/Liu Youmin) KIGALI - Fainali ya Rwanda ya Mashindano ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya "Daraja la Lugha ya Kichina" ya mwaka 2026 kwa Wanafunzi wa Vyuo na Shule za Sekondari imefanyika Kigali, mji mkuu wa nchi hiyo, Jumapili.

Watu waliovalia mavazi ya Kiafrika wakishiriki kwenye Tamasha la Utamaduni la Siku ya Afrika mjini Beijing, mji mkuu wa China, Mei 23, 2026. (Picha kwa hisani ya waandaaji/kupitia People’s Daily Online)

Mitindo ya mavazi yawa kivutio katika Tamasha la Utamaduni la Siku ya Afrika mjini Beijing, China

Jumamosi, Mei 23 Tamasha la Utamaduni la Siku ya Afrika kwa Waafrika wanaoishi China lilifanyika mjini Beijing, mji mkuu wa China likivutia watu wengi kuja kujionea utajiri wa utamaduni wa Afrika na mambo mbalimbali yanayowakilisha ushirikiano na ukaribu wa muda mrefu wa kati ya China na Afrika. Katika tamasha hilo, moja ya vivutio vikubwa ilikuwa mitindo ya mavazi ya kijadi kutoka tamaduni mbalimbali za Afrika.

Tamasha la Siku ya Afrika lafanyika Beijing likiangazia mabadilishano kati ya China na Afrika

Tamasha la wazi la Siku ya Afrika mwaka 2026 likifanyika mjini Beijing, China, Mei 23, 2026. (Picha na People’s Daily Online) Tamasha la wazi la Siku ya Afrika mwaka 2026 kwa Waafrika wanaoishi China limefanyika mjini Beijing, China juzi Jumamosi likiwaleta pamoja wanadiplomasia wanaoziwakilisha nchi mbalimbali duniani hususani za Afrika, maofisa wa serikali ya China, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa nchini China na watu wa pande mbili za China na Afrika kusherehekea utajiri wa kitamaduni wa Afrika.

Iliyopita1 2 3 4 5 6 Inayofuata