NAIROBI - Kiasi cha jumla cha mizigo kilichosafirishwa kwenye ya Reli ya Standard Gauge (SGR) ya Mombasa-Nairobi ya Kenya, mradi kinara chini ya ushirikiano wa Ukanda Mmoja, Njia Moja (BRI), kimezidi tani milioni 50 kufikia Julai 26, Kampuni ya Uendeshaji wa Reli ya Africa Star (Afristar) imesema Jumatatu. Kampuni hiyo imesema tangu kuanza kwa uendeshaji wake Mei 31, 2017, reli hiyo ya SGR ya Mombasa-Nairobi imedumisha rekodi ya uendeshaji salama kwa siku zaidi ya 3,300 mfululizo.
LUSAKA - Mirriam Chola, mwanafunzi katika Jimbo la Copperbelt la Zambia, kwa muda mrefu alikuwa akiota kuhudhuria shule ambayo anaweza kufika kwa kutembea kwa miguu kutoka nyumbani kwake huko Kalulushi, mji wa pembezoni karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. "Nilikuwa nikisoma katika shule ya Katoliki ambapo nilikuwa na changamoto ya kuwa pamoja na familia yangu, na nilikuwa nikiwakumbuka sana," Chola amekumbushia.
Tokea Mei 1, China ilianza kutekeleza sera ya ushuru-sifuri kwa bidhaa kutoka nchi 53 za Afrika ambazo inadumisha uhusiano wa kidiplomasia nazo. Kwa mujibu wa Kampuni ya Uendeshaji wa Reli ya Africa Star, Reli ya SGR ya Kenya iliendesha treni za mizigo jumla ya 3,931 katika nusu ya kwanza ya mwaka 2026, ikisafirisha tani milioni 4.
Usiku unapoingia katika mji wa Shenzhen, Mkoa wa Guangdong, China, malori yaliyosheheni matunda freshi yanapita kwa kasi barabarani, yakipeleka matunda matamu kutoka Afrika Kusini kwenye supamaketi na masoko sehemu mbali mbali nchini China. “Kwa ushuru wa forodha kushuka kutoka asilimia 10 hadi sifuri, gharama za uagizaji kwa shehena hii ya tufaha imepungua kwa karibu Yuan 20,000," amesema Luo Shengcong, Meneja Mkuu wa Kampuni ya Kimataifa ya Usafirishaji wa Mizigo ya Jianchengye ya Shenzhen.