NAIROBI – Siku ya 17 ya Lugha ya Kichina ya Umoja wa Mataifa kwa mwaka huu wa 2026 imesherehekewa jana Jumatatu jijini Nairobi, Kenya, kwa wito wa kuhimiza mazungumzo kati ya tamaduni na ustaarabu mbalimbali. Shughuli hiyo ilifanyika katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa jijini Nairobi (UNON) chini ya kaulimbiu ya "Lugha ya Kichina Hudumu, Ustaarabu Hung'aa," ambapo wanadiplomasia, wasomi, na wanafunzi walikusanyika pamoja na kuhimiza mazungumzo na maelewano duniani.
(Picha/Xinhua) Jukwaa la Biashara kati ya Kenya na China limefanyika jana Jumatatu katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, likilenga kuimarisha uhusiano wa biashara na uwekezaji kati ya nchi hizo mbili chini ya sera ya ushuru-sifuri ya China itakayoanza kutekelezwa Mei Mosi mwaka huu. Mkutano huo ulihudhuriwa na Naibu Rais wa Kenya Kithure Kindiki na Makamu wa Rais wa China Han Zheng ambao waliongoza ujumbe wa maofisa wa ngazi ya juu wa Kenya na China, na wafanyabiashara wakuu na wamiliki wa viwanda kutoka nchi zote mbili.
Yakiwa ni maziwa makubwa zaidi ya maji freshi nchini China na Afrika, mtawalia, Ziwa Poyang na Ziwa Victoria yameshuhudia ushirikiano wa kuvuka bara kwa ajili ya maendeleo endelevu na uhifadhi wa ikolojia. Ziwa Victoria ni hifadhi kuu ya Mto Nile, na Ziwa Poyang linaungana na Mto Yangtze wa China.
Wakazi wenyeji wakichukua maji safi kwenye bomba la umma lililowekwa chini ya mradi wa maji safi unaosaidiwa na China huko Chaani, Zanzibar, Tanzania, Machi 22, 2026. (Xinhua/Emmanuel Herman) ZANZIBAR - Shukrani na matumaini sasa ni sehemu ya maisha ya kila siku kwa Juma Makame Mohamed na Huzaima Bakari Haji, wakazi wawili wa Chaani ambao jamii yao imebadilishwa na mradi wa maji safi unaoungwa mkono na China.