Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar, Christine Razanamahasoa, anatoa hotuba kwenye hafla za vyakula vitamu vya China kwa kusherehekea Mwaka Mpya wa Jadi wa China mjini Antananarivo, Madagascar, Februari 7, 2026. (Picha na Sitraka Rajaonarison/Xinhua) Waziri wa Mambo ya nje wa Madagascar Christine Razanamahasoa amesema anatarajia uhusiano kati ya nchi hiyo na China utaonesha uhai mpya katika mwaka mpya, na pia ametoa salamu za Mwaka Mpya wa Jadi wa China kwa watu wa China.
Mgeni Mtanzania na mtoto wa China wakijaribu kuandika maandiko ya Kichina kwenye Ubalozi wa China huko Dar es Salaam, Tanzania, Februari 6, 2026. (Xinhua/Emmanuel Herman) DAR ES SALAAM, Februari 7 -- Watanzania na Wachina wanaoishi Tanzania walikusanyika katika Ubalozi wa China nchini Tanzania Ijumaa iliyopita wakisherehekea pamoja Sikukuu inayokaribia ya Mwaka Mpya wa Jadi wa China.
Wanafunzi wa Tanzania wakijifunza kupika baozi kwa mvuke huko Dar es Salaam, Tanzania, Januari 28, 2026. (Xinhua/Emmanuel Herman) DAR ES SALAAM – Ndani ya jiko lenye pilikapilika nyingi katikati ya jiji la Dar es Salaam, Ruth Washima Seni, mwanafunzi kijana wa mambo ya hoteli nchini Tanzania, anajaribu kukata viazi mviringo katika vipande vyembamba kama nywele.
Picha hii ya kumbukumbu isiyo na tarehe ikionyesha mandhari ya Kituo cha Kuzalisha Umeme kwa Nishati ya Upepo cha Aysha II katika Jimbo la Somali, Ethiopia. (Kampuni ya Umeme ya Dongfang/kupitia Xinhua) ADDIS ABABA - Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed Jumamosi alizindua mradi wa kipindi cha kwanza wa Kituo cha Kuzalisha Umeme kwa Nishati ya Upepo cha Aysha II katika Jimbo la Somali, akisisitiza kwamba maendeleo ya nishati safi ni kiini cha kazi ya muda mrefu ya kubadilisha mundo wa uchumi wa nchi hiyo.