Ongezeko la watalii Wachina wanaowasili Zimbabwe linachochea hitaji la wataalamu wanaoongea lugha ya Kichina na kutoa fursa mpya za ajira katika sekta za utalii na huduma, wakati ambapo mapumziko ya siku 5 nchini China ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yakimalizika jana Jumanne. Mwongoza watalii na mwanzilishi wa kampuni ya ushauri wa Lugha ya Zimgro Tawanda Zimhindo amesema, idadi kubwa ya watalii kutoka China imelazimisha kuboresha ufanisi wa lugha kwa waongoza watalii na wafanyakazi wa hoteli.
LOME - Togo Jumatatu ilifanya gwaride kubwa la kijeshi na maandamano ya raia kusherehekea miaka 66 tangu kupata uhuru wake. Rais wa Togo Jean-Lucien Savi de Tove, Rais wa Baraza la Mawaziri Faure Gnassingbe, pamoja na viongozi wengine, wawakilishi kutoka sekta mbalimbali na wajumbe wa kundi la wanadiplomasia, walihudhuria hafla hiyo.
Kisiwa cha Gulangyu, "Bustani ya Baharini" ya kuvutia karibu na pwani ya Xiamen, Mkoa wa Fujian, kusini mashariki mwa China, kwa muda mrefu kimekuwa mahali pa kukutana tamaduni, ambako historia, muziki na maisha ya kila siku huchangamana katika mazingira ya kipekee ya ushairi. Hivi karibuni, Aris, kutoka Tanzania, alisafiri akiwa na picha ya Tingatinga kutoka nchi yake kwenda katika kisiwa hicho na kuanza safari ya kipekee ya biashara ya kubadilishana vitu kwa vitu na mabadilishano kwenye kisiwa hicho.
KIGALI - Kwenye mashamba yenye rutuba ya Kijiji cha Ibiza, Wilaya ya Kayonza mashariki mwa Rwanda, safu za pilipili nyekundu zilizostawi ni zaidi ya zao la kuuzwa nje -- zinabadilisha maisha. Kwa mamia ya wakulima katika wilaya hiyo ya Kayonza, mauzo ya nje ya pilipili yanayozidi kuongezeka ya Rwanda kwenda China yanafungua njia ya kutoka katika umaskini, yakichochewa na sera ya ushuru-sifuri ya China na mahitaji makubwa ya soko la China.