Jumamosi, Mei 23 Tamasha la Utamaduni la Siku ya Afrika kwa Waafrika wanaoishi China lilifanyika mjini Beijing, mji mkuu wa China likivutia watu wengi kuja kujionea utajiri wa utamaduni wa Afrika na mambo mbalimbali yanayowakilisha ushirikiano na ukaribu wa muda mrefu wa kati ya China na Afrika. Katika tamasha hilo, moja ya vivutio vikubwa ilikuwa mitindo ya mavazi ya kijadi kutoka tamaduni mbalimbali za Afrika.
Tamasha la wazi la Siku ya Afrika mwaka 2026 likifanyika mjini Beijing, China, Mei 23, 2026. (Picha na People’s Daily Online) Tamasha la wazi la Siku ya Afrika mwaka 2026 kwa Waafrika wanaoishi China limefanyika mjini Beijing, China juzi Jumamosi likiwaleta pamoja wanadiplomasia wanaoziwakilisha nchi mbalimbali duniani hususani za Afrika, maofisa wa serikali ya China, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa nchini China na watu wa pande mbili za China na Afrika kusherehekea utajiri wa kitamaduni wa Afrika.
(Picha/Xinhua) Mazungumzo kati ya vijana wa China na Afrika yamefanyika Alhamis katika mji wa Pretoria, Afrika Kusini, na kukutanisha wawakilishi wa vijana waliobadilishana maoni kuhusu uhusiano wa pande mbili, ushirikiano wa Kusini na Kusini, maendeleo ya vijana na ushirikiano wa pande nyingi. Chini ya kaulimbiu "Ushirikiano wa Kusini na Kusini katika Dunia ya Pande Nyingi," washiriki walisema ushiriki wa vijana una umuhimu mkubwa katika kuunda ushirikiano duniani.
Kuanzia tarehe Mosi, Mei, China imeanza kutekeleza sera ya kutotoza ushuru kwa nchi zote 53 za Afrika zenye uhusiano wa kidiplomasia nayo. Hatua hiyo ya China imechukuliwa kuwa hatua muhimu kwa kuhimiza ufunguaji mlango na ushirikiano kati ya nchi za Dunia ya Kusini, wakati hali ya kujilinda na kuparaganyika kiuchumi inazidi kuonekana duniani kote.