ADDIS ABABA - Maafisa kutoka China na Umoja wa Afrika (AU) wamesisitiza umuhimu wa Maonyesho ya Uagizaji na Uuzaji Nje Bidhaa ya China, ambayo pia yanajulikana kwa jina la Maonyesho ya Canton, katika kuunganisha biashara za Afrika na wanunuzi, wawekezaji, washirika wa teknolojia, na fursa mpya za kibiashara duniani. Kauli hiyo imetolewa kwenye mkutano uliofanyika Jumanne wiki hii katika makao makuu ya AU mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, ili kutangaza Maonyesho ya 140 ya Canton.
Kutimiza mambo ya kisasa imekuwa ni jitihada isiyokoma ya watu wa China tangu zama za karibuni, na pia ni matarajio ya pamoja ya watu wa mataifa yote duniani. "China imeweza kufanikiwa, na nchi zingine zinazoendelea zinaweza kufanikiwa vilevile.
PRETORIA, Afrika Kusini - Kampuni ya kuunda magari ya Chery ya China imezindua rasmi kiwanda chake cha kuzalisha magari siku ya Ijumaa huko Rosslyn, kaskazini mwa mji mkuu wa utawala wa Afrika Kusini, Pretoria, ikiashiria mabadiliko yake ya kuwa mzalishaji magari wa nchini humo na kuzidisha dhamira yake ya muda mrefu kwa soko la Afrika Kusini. Akihutubia hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho, Mwenyekiti wa Chery Yin Tongyue amesema uwekezaji huo unaonyesha dhamira ya muda mrefu ya kampuni hiyo kwa Afrika Kusini.
Waziri wa Utalii na Utamaduni wa Ushelisheli Amanda Bernstein akizungumza kwenye mahojiano na Shirika la Habari la China, Xinhua mjini Victoria,Ushelisheli, Juni 25, 2026. (Xinhua/Xie Jianfei) VICTORIA - Waziri wa Utalii na Utamaduni wa Ushelisheli Amanda Bernstein amesema uhusiano kati ya Ushelisheli na China sasa unaingia katika zama mpya ya ushirikiano na maendeleo, hasa katika mawasiliano ya kitamaduni.