KINSHASA - Jukwaa la Vyombo vya Habari la China na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) chini ya kaulimbiu ya "Mambo ya Kisasa ya China na Njia ya Maendeleo ya DRC: Kuchunguza kwa Pamoja Njia Mpya kwa ajili ya Kunufaishana na Ushirikiano wenye Mafanikio kwa Pande Zote," limefanyika jana Jumatano mjini Kinshasa, mji mkuu wa DRC. Jukwaa hilo limevutia wanasiasa, wawakilishi wa vyombo vya habari na viongozi wa kibiashara wapatao 250 kutoka nchi zote mbili.
Balozi wa zamani wa Ghana nchini China Bw. Anani Demuyakor amezisifu Ghana na China kwa kuendelea kuimarisha uhusiano wao, wa pande mbili kwa kusisitiza zaidi juu ya mabadilishano kati ya watu na watu na masuala ya maendeleo.
Mashindao ya 7 ya Wushu Kung Fu ya Vijana ya Afrika yamefunguliwa Jumanne wiki hii katika mji mkuu wa Misri, Cairo, na kukutanisha wanamichezo, makocha, na maofisa karibu 100 kutoka nchi mbalimbali za Afrika pamoja Timu ya Taifa ya Wushu ya China. Akizungumza kwenye uzinduzi wa mashindano hayo, Rais wa Shirikisho ya Wushu Kung Fu la Afrika, Sherif Mostafa amesema, mchezo huo unazingatia amani na nidhamu binafsi na kwamba mashindano hayo yanatumika kama jukwaa la maendeleo ya vijana na pia kama daraja kati ya urithi wa Afrika na sanaa ya Kung Fu ya China.
Uganda imezindua Mwaka wa Mawasiliano ya Watu na Watu kati ya China na Uganda wakati wa tamasha lililofanyika mjini Kampala, mji mkuu wa Uganda hapo jana Jumapili, kusherehekea Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Jadi wa China. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Makamu wa rais wa Uganda Jessica Alupo amesema ushirikiano kati ya China na Uganda umekuwa ni wa kunufaishana, na kuishukuru China kwa kuunga mkono maendeleo ya miundombinu nchini Uganda, ufadhili wa masomo, na miradi ya kujenga uwezo.