Kongamano la ngazi ya juu kuhusu Maonesho ya 9 ya Uagizaji Bidhaa ya Kimataifa ya China (CIIE) na Jukwaa la tisa la Uchumi la Kimataifa la Hongqiao (HQF) lilifanyika Jumanne katika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, likisisitiza haja ya kutumia vizuri majukwaa haya "maalum na yenye nguvu" ili kuingia kwenye soko kubwa la China na kuharakisha ukuaji wa viwanda barani Afrika. Kongamano hilo la ngazi ya juu liliandaliwa kwa pamoja na Idara ya CIIE na Sekritarieti ya Jukwaa la Hongqiao, kwa ushirikiano na Ujumbe wa China katika Umoja wa Afrika na Kamisheni ya umoja huo.
Aprili 12, maonyesho ya "Kufunzana kati ya Ustaarabu" — Maonyesho ya Sanaa za Vinyago vya Afrika kutoka kwenye ukusanyaji wa Jumba la Makumbusho ya Sanaa ya Kitaifa ya China" yalifunguliwa kwenye Jumba la Makumbusho ya Sanaa ya Kitaifa ya China mjini Beijing. Yakiwa ni mradi muhimu wa "Mwaka wa Mawasiliano ya Kitamaduni kati ya Watu wa China na Afrika 2026," maonyesho hayo yanaandaliwa kwa ushirikiano na Jumuiya ya China kwa ajili ya Mabadilishano ya Kitamaduni na Nchi za Nje na Jumba la Makumbusho ya Sanaa ya Kitaifa ya China.
NAIROBI – Siku ya 17 ya Lugha ya Kichina ya Umoja wa Mataifa kwa mwaka huu wa 2026 imesherehekewa jana Jumatatu jijini Nairobi, Kenya, kwa wito wa kuhimiza mazungumzo kati ya tamaduni na ustaarabu mbalimbali. Shughuli hiyo ilifanyika katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa jijini Nairobi (UNON) chini ya kaulimbiu ya "Lugha ya Kichina Hudumu, Ustaarabu Hung'aa," ambapo wanadiplomasia, wasomi, na wanafunzi walikusanyika pamoja na kuhimiza mazungumzo na maelewano duniani.
(Picha/Xinhua) Jukwaa la Biashara kati ya Kenya na China limefanyika jana Jumatatu katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, likilenga kuimarisha uhusiano wa biashara na uwekezaji kati ya nchi hizo mbili chini ya sera ya ushuru-sifuri ya China itakayoanza kutekelezwa Mei Mosi mwaka huu. Mkutano huo ulihudhuriwa na Naibu Rais wa Kenya Kithure Kindiki na Makamu wa Rais wa China Han Zheng ambao waliongoza ujumbe wa maofisa wa ngazi ya juu wa Kenya na China, na wafanyabiashara wakuu na wamiliki wa viwanda kutoka nchi zote mbili.