Kenya inaongeza juhudi ili kuendeleza sekta yake ya filamu kwa kutafuta uwekezaji na ushirikiano na wawekezaji wa China. Mwenyekiti wa Kamisheni ya Filamu ya Kenya Bw.
Matumizi ya nishati ya kijani barani Afrika yameongezeka kwa kasi kutokana na upatikanaji wa suluhisho la bidhaa za ubora wa juu na gharama nafuu za umeme wa jua zinazotengenezwa nchini China. Meneja wa mradi katika Kituo cha Uwezo wa Nishati, Mazingira na Uchumi Endelevu katika Kampuni ya Huduma ya AHK East Africa, Georg Pflomm amesema, bidhaa zinazotumia nishati ya jua zinazotengenezwa nchini China zimeboresha upatikanaji wa nishati na usalama katika bara la Afrika linalotaka kuendeleza utoaji mdogo wa hewa ya kaboni.
Ubalozi wa China nchini Sudan Kusini umetoa msaada wa zaidi ya vifaa 20 vya mashine za kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula katika mkoa wa Ikweta Magharibi nchini humo. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo hapo jana, msaidizi wa katibu mkuu wa Wizara ya Ujenzi wa Amani Pia Philip Michael amesema, vifaa hivyo vitaboresha usalama wa chakula na kusaidia juhudi za ujenzi wa amani katika mkoa huo ambao umeshuhudia mapigano ya kikabila tangu mwaka 2021.
Mjumbe Maalum wa Rais Xi Jinping wa China ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge la Umma la China Bw. Zheng Jianbang amehudhuria hafla ya kuapishwa kwa Rais mpya wa Guinea, Mamady Doumbouya iliyofanyika Conakry, mji mkuu wa nchi hiyo juzi Jumamosi na kufanya mazungumzo naye.