ZANZIBAR - Asubuhi ya Jumamosi yenye mwanga angavu huko Kombeni, nje kidogo ya Jiji la Zanzibar, Tanzania, mfanyakazi wa ulinzi mwenye umri wa miaka 71 Amin Maulid Juma alitoka kwenye Kliniki ya Sinai akiwa na hisia mpya ya unafuu na shukrani. Kwa wiki kadhaa, alikuwa amevumilia usiku mfululizo wa kukosa usingizi kutokana na maumivu ya tumbo yasiyokoma.
DAR ES SALAAM - Saluni ya kitamaduni iliyofanyika Jumapili jioni jijini Dar es Salaam, Tanzania iliwaleta pamoja wasanii kutoka China na Tanzania na kuonyesha dhahiri ubadilishanaji wa kistaarabu unaolenga kuzidisha uhusiano wa kitamaduni kati ya nchi hizo mbili. Shughuli hiyo, iliyoandaliwa na Ubalozi wa China nchini Tanzania, Kituo cha China cha Ubadilishanaji wa Kimataifa wa Kitamaduni na Kuhimiza Utalii nchini Tanzania, iliwaleta pamoja maafisa wa serikali, wasomi, wasanii, na wajumbe wa jumuiya ya Wachina nchini Tanzania.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China Miao Deyu akihudhuria na kutoa hotuba kwenye hafla iliyoandaliwa na Kundi la Mabalozi wa Afrika nchini China kusherehekea "Siku ya Afrika" mjini Beijing, Mei 25, 2026. (CMFA/People’s Daily Online) Kundi la Mabalozi wa Afrika nchini China (GAAC) limeandaa hafla ya mapokezi ya kidiplomasia ya ngazi ya juu jana Jumatatu jioni mjini Beijing kuadhimisha Siku ya Afrika 2026, ikiwakutanisha Wakuu wa Balozi na wanadiplomasia wa Afrika, mabalozi kutoka makundi mengine ya kikanda, maofisa waandamizi wa Serikali ya China, mawaziri wa Afrika walioko ziarani China, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, wajumbe wa diaspora wa Afrika, viongozi wa kibiashara, wasomi, na marafiki wa muda mrefu wa Afrika nchini China.
Nkurunziza Tharcisse, mshindi wa fainali ya Rwanda ya Mashindano ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya "Daraja la Lugha ya Kichina" ya mwaka 2026 kwa Wanafunzi wa Vyuo, akipiga picha na Gao Wenqi, Balozi wa China nchini Rwanda, mjini Kigali, Rwanda, Mei 24, 2026. (Xinhua/Liu Youmin) KIGALI - Fainali ya Rwanda ya Mashindano ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya "Daraja la Lugha ya Kichina" ya mwaka 2026 kwa Wanafunzi wa Vyuo na Shule za Sekondari imefanyika Kigali, mji mkuu wa nchi hiyo, Jumapili.