人民网首页

Habari

Mashindano ya Wushu ya China na Afrika yafunguliwa nchini Misri

Mashindao ya 7 ya Wushu Kung Fu ya Vijana ya Afrika yamefunguliwa Jumanne wiki hii katika mji mkuu wa Misri, Cairo, na kukutanisha wanamichezo, makocha, na maofisa karibu 100 kutoka nchi mbalimbali za Afrika pamoja Timu ya Taifa ya Wushu ya China. Akizungumza kwenye uzinduzi wa mashindano hayo, Rais wa Shirikisho ya Wushu Kung Fu la Afrika, Sherif Mostafa amesema, mchezo huo unazingatia amani na nidhamu binafsi na kwamba mashindano hayo yanatumika kama jukwaa la maendeleo ya vijana na pia kama daraja kati ya urithi wa Afrika na sanaa ya Kung Fu ya China.

Uganda yafanya tamasha la kusherehekea mawasiliano ya watu na watu wakati Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Jadi wa China ikikaribia

Uganda imezindua Mwaka wa Mawasiliano ya Watu na Watu kati ya China na Uganda wakati wa tamasha lililofanyika mjini Kampala, mji mkuu wa Uganda hapo jana Jumapili, kusherehekea Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Jadi wa China. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Makamu wa rais wa Uganda Jessica Alupo amesema ushirikiano kati ya China na Uganda umekuwa ni wa kunufaishana, na kuishukuru China kwa kuunga mkono maendeleo ya miundombinu nchini Uganda, ufadhili wa masomo, na miradi ya kujenga uwezo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar atarajia uhusiano kati ya nchi hiyo na China kuonesha uhai mpya katika mwaka mpya

Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar, Christine Razanamahasoa, anatoa hotuba kwenye hafla za vyakula vitamu vya China kwa kusherehekea Mwaka Mpya wa Jadi wa China mjini Antananarivo, Madagascar, Februari 7, 2026. (Picha na Sitraka Rajaonarison/Xinhua) Waziri wa Mambo ya nje wa Madagascar Christine Razanamahasoa amesema anatarajia uhusiano kati ya nchi hiyo na China utaonesha uhai mpya katika mwaka mpya, na pia ametoa salamu za Mwaka Mpya wa Jadi wa China kwa watu wa China.

Watanzania na Wachina wanaoishi Tanzania washerehekea Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Jadi wa China mjini Dar es Salaam

Mgeni Mtanzania na mtoto wa China wakijaribu kuandika maandiko ya Kichina kwenye Ubalozi wa China huko Dar es Salaam, Tanzania, Februari 6, 2026. (Xinhua/Emmanuel Herman) DAR ES SALAAM, Februari 7 -- Watanzania na Wachina wanaoishi Tanzania walikusanyika katika Ubalozi wa China nchini Tanzania Ijumaa iliyopita wakisherehekea pamoja Sikukuu inayokaribia ya Mwaka Mpya wa Jadi wa China.

Iliyopita5 6 7 8 9 10 Inayofuata