人民网首页

Habari

China na Lesotho zaapa kusukuma mbele ushirikiano wa kimkakati hadi ngazi ya juu zaidi

(Picha inatoka tovuti ya Wizara ya Mambo ya Nje ya China.) Lesotho na China zimethibitisha tena dhamira yao ya kusukuma mbele ushirikiano wa kimkakati wa pande mbili hadi ngazi ya juu na kuufanya kuwa mfano wa mawasiliano ya kirafiki na maendeleo ya pamoja kati ya nchi zenye hali na mifumo tofauti ya kitaifa.

Kuadhimisha miaka 70 ya uhusiano wa kidiplomasia, China na Afrika zaimarisha ushirikiano katika kusukuma mbele mambo ya kisasa

Hafla ya uzinduzi wa Mwaka wa 2026 wa Mawasiliano kati ya Watu wa China na Afrika ikifanyika kwenye makao makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, Januari 8, 2026. (Xinhua/Han Xu) JOHANNESBURG - Mwaka huu unatimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Afrika.

China na Umoja wa Afrika zafanya mazungumzo ya kimkakati katika makao makuu ya AU

Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi, ambaye pia ni Mjumbe wa Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Mahmoud Ali Youssouf wakifanya kwa pamoja Mazungumzo ya tisa ya Kimkakati kati ya China na AU kwenye makao makuu ya AU mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, Januari 8, 2026. (Xinhua/Han Xu) Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Mahmoud Ali Youssouf kwa pamoja wamefanya Mazungumzo ya 9 ya Kimkakati kati ya China na AU kwenye makao makuu ya Umoja huo mjini Addis Ababa, Ethiopia.

China, Ethiopia zaahidi kutekeleza matokeo ya mkutano wa kilele wa FOCAC wa Beijing

Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi jana Alhamisi alikutana na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed na Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Gedion Timothewos mjini Addis Ababa, huku pande hizo mbili zikiahidi kusukuma mbele kwa pamoja utekelezaji wa matokeo yaliyopatikana kwenye Mkutano wa Kilele wa Beijing wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa kwa wanahabari, pande hizo mbili zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika nyanja zote na kujitahidi kujenga uhusiano wa kimkakati wa hali zote kati ya China na Ethiopia kuwa mfano wa kuigiwa kwa ajili ya kujenga Jumuiya ya hali zote ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja katika zama mapya.

Iliyopita3 4 5 6 7