人民网首页

Habari

Sera ya Ushuru-Sifuri Yasaidia Bidhaa Bora za Afrika Kukumbatia Soko Kubwa la China

Maofisa wa Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun wakifanya ukaguzi wa maparachichi freshi kutoka Kenya baada ya sera ya ushuru-sifuri kwa nchi 53 zenye uhusiano wa kidiplomasia na China kuanza kutekelezwa, Mei 1, 2026. (Picha kwa hisani ya Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun) Tufaha freshi kutoka Afrika Kusini, machungwa freshi ya Misri, maparachichi freshi ya Kenya.

Daktari mchina bingwa wa mfumo wa mkojo Wang Kunpeng (kulia) na mhudumu wa afya mwenyeji (kushoto) wakipiga picha na mgonjwa Selemani Juma Selemani baada ya upasuaji katika Hospitali ya Lumumba, Zanzibar, Tanzania, Januari 26, 2026. (Kundi la 35 la Timu ya madaktari Wachina visiwani Zanzibar/kupitia Xinhua)

Upasuaji wa kuokoa maisha Zanzibar waakisi ushirikiano unaokua wa afya kati ya China na Tanzania

ZANZIBAR, Tanzania - Kwa miaka mitano, Selemani Juma Selemani Mtanzania mwenye umri wa miaka 24 amekuwa akiishi na hali ya maumivu, homa, na kukosa utulivu kwa kudumu kutokana na hali ngumu ya mfumo wa mkojo ambayo imekuwa ikimsumbua maisha yake ya kila siku. Akiwa ni mfanyakazi wa hoteli katika Kisiwa cha Unguja, Zanzibar, Tanzania, Selemani alikuwa akihangaika kudumisha utaratibu wa kawaida.

Zimbabwe yajipanga kuimarisha utalii wakati idadi ya watalii kutoka China ikiongezeka

Ongezeko la watalii Wachina wanaowasili Zimbabwe linachochea hitaji la wataalamu wanaoongea lugha ya Kichina na kutoa fursa mpya za ajira katika sekta za utalii na huduma, wakati ambapo mapumziko ya siku 5 nchini China ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yakimalizika jana Jumanne. Mwongoza watalii na mwanzilishi wa kampuni ya ushauri wa Lugha ya Zimgro Tawanda Zimhindo amesema, idadi kubwa ya watalii kutoka China imelazimisha kuboresha ufanisi wa lugha kwa waongoza watalii na wafanyakazi wa hoteli.

Kikundi cha utamaduni wa jadi wa China kinachoundwa na wanafunzi kutoka Taasisi ya Confucius katika Chuo Kikuu cha Lome kikishiriki kwenye gwaride la Siku ya Uhuru wa Togo, Lome, Togo, Aprili 27, 2026. (Xinhua/Si Yuan)

Utamaduni wa jadi wa China waonekana kwa mara ya kwanza kwenye sherehe za Siku ya Uhuru wa Togo

LOME - Togo Jumatatu ilifanya gwaride kubwa la kijeshi na maandamano ya raia kusherehekea miaka 66 tangu kupata uhuru wake. Rais wa Togo Jean-Lucien Savi de Tove, Rais wa Baraza la Mawaziri Faure Gnassingbe, pamoja na viongozi wengine, wawakilishi kutoka sekta mbalimbali na wajumbe wa kundi la wanadiplomasia, walihudhuria hafla hiyo.

Iliyopita5 6 7 8 9 10 Inayofuata