人民网首页

Picha

Picha hii iliyopigwa tarehe 23, Machi, 2026 ikionesha treni ya mizigo ikiegesha kwenye Stesheni ya Nairobi ya Reli ya Mombasa-Nairobi. (Picha na Nelson Asienwa/Xinhua)

Sera ya kutotoza ushuru yahimiza mchakato wa maendeleo ya mambo ya kisasa ya China na Afrika

Kuanzia tarehe Mosi, Mei, China imeanza kutekeleza sera ya kutotoza ushuru kwa nchi zote 53 za Afrika zenye uhusiano wa kidiplomasia nayo. Hatua hiyo ya China imechukuliwa kuwa hatua muhimu kwa kuhimiza ufunguaji mlango na ushirikiano kati ya nchi za Dunia ya Kusini, wakati hali ya kujilinda na kuparaganyika kiuchumi inazidi kuonekana duniani kote.

Sera ya Ushuru-Sifuri Yasaidia Bidhaa Bora za Afrika Kukumbatia Soko Kubwa la China

Maofisa wa Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun wakifanya ukaguzi wa maparachichi freshi kutoka Kenya baada ya sera ya ushuru-sifuri kwa nchi 53 zenye uhusiano wa kidiplomasia na China kuanza kutekelezwa, Mei 1, 2026. (Picha kwa hisani ya Forodha ya Uwanja wa Ndege wa Guangzhou Baiyun) Tufaha freshi kutoka Afrika Kusini, machungwa freshi ya Misri, maparachichi freshi ya Kenya.

Kikundi cha utamaduni wa jadi wa China kinachoundwa na wanafunzi kutoka Taasisi ya Confucius katika Chuo Kikuu cha Lome kikishiriki kwenye gwaride la Siku ya Uhuru wa Togo, Lome, Togo, Aprili 27, 2026. (Xinhua/Si Yuan)

Utamaduni wa jadi wa China waonekana kwa mara ya kwanza kwenye sherehe za Siku ya Uhuru wa Togo

LOME - Togo Jumatatu ilifanya gwaride kubwa la kijeshi na maandamano ya raia kusherehekea miaka 66 tangu kupata uhuru wake. Rais wa Togo Jean-Lucien Savi de Tove, Rais wa Baraza la Mawaziri Faure Gnassingbe, pamoja na viongozi wengine, wawakilishi kutoka sekta mbalimbali na wajumbe wa kundi la wanadiplomasia, walihudhuria hafla hiyo.

Mkulima Deborah Muhawenimana akipiga picha akiwa na pilipili freshi iliyochumwa punde katika Kijiji cha Ibiza cha Wilaya ya Kayonza katika Mkoa wa Mashariki, Rwanda, Aprili 14, 2026. (Xinhua/Ju Yinhe)

Sera ya Ushuru-sifuri ya China yabadilisha maisha ya wakulima wa pilipili wa Rwanda

KIGALI - Kwenye mashamba yenye rutuba ya Kijiji cha Ibiza, Wilaya ya Kayonza mashariki mwa Rwanda, safu za pilipili nyekundu zilizostawi ni zaidi ya zao la kuuzwa nje -- zinabadilisha maisha. Kwa mamia ya wakulima katika wilaya hiyo ya Kayonza, mauzo ya nje ya pilipili yanayozidi kuongezeka ya Rwanda kwenda China yanafungua njia ya kutoka katika umaskini, yakichochewa na sera ya ushuru-sifuri ya China na mahitaji makubwa ya soko la China.

1 2 3 4 下一页