人民网首页

Picha

Mkulima Deborah Muhawenimana akipiga picha akiwa na pilipili freshi iliyochumwa punde katika Kijiji cha Ibiza cha Wilaya ya Kayonza katika Mkoa wa Mashariki, Rwanda, Aprili 14, 2026. (Xinhua/Ju Yinhe)

Sera ya Ushuru-sifuri ya China yabadilisha maisha ya wakulima wa pilipili wa Rwanda

KIGALI - Kwenye mashamba yenye rutuba ya Kijiji cha Ibiza, Wilaya ya Kayonza mashariki mwa Rwanda, safu za pilipili nyekundu zilizostawi ni zaidi ya zao la kuuzwa nje -- zinabadilisha maisha. Kwa mamia ya wakulima katika wilaya hiyo ya Kayonza, mauzo ya nje ya pilipili yanayozidi kuongezeka ya Rwanda kwenda China yanafungua njia ya kutoka katika umaskini, yakichochewa na sera ya ushuru-sifuri ya China na mahitaji makubwa ya soko la China.

(Picha/Xinhua)

Kongamano kuhusu Maonesho ya 9 ya CIIE na Jukwaa la Hongqiao latoa mwito wa kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya China na Afrika

Kongamano la ngazi ya juu kuhusu Maonesho ya 9 ya Uagizaji Bidhaa ya Kimataifa ya China (CIIE) na Jukwaa la tisa la Uchumi la Kimataifa la Hongqiao (HQF) lilifanyika Jumanne katika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia, likisisitiza haja ya kutumia vizuri majukwaa haya "maalum na yenye nguvu" ili kuingia kwenye soko kubwa la China na kuharakisha ukuaji wa viwanda barani Afrika. Kongamano hilo la ngazi ya juu liliandaliwa kwa pamoja na Idara ya CIIE na Sekritarieti ya Jukwaa la Hongqiao, kwa ushirikiano na Ujumbe wa China katika Umoja wa Afrika na Kamisheni ya umoja huo.

"Kufunzana kati ya Ustaarabu"—Maonyesho ya Vinyago vya Afrika.

"Kufunzana kati ya Ustaarabu" - Maonyesho ya Vinyago vya Afrika Yafanyika Beijing, China

Aprili 12, maonyesho ya "Kufunzana kati ya Ustaarabu" — Maonyesho ya Sanaa za Vinyago vya Afrika kutoka kwenye ukusanyaji wa Jumba la Makumbusho ya Sanaa ya Kitaifa ya China" yalifunguliwa kwenye Jumba la Makumbusho ya Sanaa ya Kitaifa ya China mjini Beijing. Yakiwa ni mradi muhimu wa "Mwaka wa Mawasiliano ya Kitamaduni kati ya Watu wa China na Afrika 2026," maonyesho hayo yanaandaliwa kwa ushirikiano na Jumuiya ya China kwa ajili ya Mabadilishano ya Kitamaduni na Nchi za Nje na Jumba la Makumbusho ya Sanaa ya Kitaifa ya China.

Wasanii wakifanya onyesho kwenye shughuli ya Siku ya Lugha ya Kichina ya Umoja wa Mataifa katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa, Nairobi (UNON) nchini Kenya, Aprili 13, 2026. (Xinhua/Liu Qiong)

Siku ya Lugha ya Kichina ya UN yaadhimishwa nchini Kenya kwa wito wa mazungumzo ya kistaarabu

NAIROBI – Siku ya 17 ya Lugha ya Kichina ya Umoja wa Mataifa kwa mwaka huu wa 2026 imesherehekewa jana Jumatatu jijini Nairobi, Kenya, kwa wito wa kuhimiza mazungumzo kati ya tamaduni na ustaarabu mbalimbali. Shughuli hiyo ilifanyika katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa jijini Nairobi (UNON) chini ya kaulimbiu ya "Lugha ya Kichina Hudumu, Ustaarabu Hung'aa," ambapo wanadiplomasia, wasomi, na wanafunzi walikusanyika pamoja na kuhimiza mazungumzo na maelewano duniani.

1 2 3 下一页