Kikao cha kufungua mkutano wa nne wa Bunge la 14 la Umma la China (NPC) kikifanyika kwenye Jumba la Mikutano ya Umma mjini Beijing, mji mkuu wa China, Machi 5, 2026. (Xinhua/Wang Ye) BEIJING - Bunge la 14 la Umma la China, chombo cha juu cha utungaji sheria cha China, limefungua mkutano wake wa nne leo Alhamisi asubuhi kwenye Jumba la Mikutano ya Umma la Beijing.
BEIJING - Bunge la 14 la Umma la China (NPC), chombo cha utungaji sheria cha China, limefanya mkutano na waandishi wa habari jana Jumatano, siku moja kabla ya kufunguliwa kwa mkutano wake wa mwaka. Lou Qinjian, msemaji wa mkutano huo wa nne wa Bunge la 14 la Umma, aliwaelezea waandishi wa habari juu ya hali ya mkutano huo.
Mkutano wa nne wa Kamati ya Kitaifa ya 14 ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la Umma la China (CPPCC) ukifunguliwa katika Jumba la Mikutano ya Umma la Beijing, Machi 4, 2026. (Xinhua/Yan Yan) BEIJING - Kamati ya Kitaifa ya 14 ya Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la Umma la China (CPPCC), chombo cha juu cha mashauri ya kisiasa cha China, imefanya mkutano wake wa nne wa mwaka kuanzia jana Jumatano mjini Beijing ambapo Rais Xi Jinping na viongozi wengine wa Chama na serikali, wakiwemo Li Qiang, Zhao Leji, Cai Qi, Ding Xuexiang, Li Xi na Han Zheng, walihudhuria kwenye ufunguzi wa mkutano huo katika Jumba la Mikutano ya Umma la Beijing.
Zhao Leji, mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge la Umma la China akiongoza kikao cha maandalizi ya mkutano wa nne wa Bunge hilo la 14 kwenye Jumba la Mikutano ya Umma la Beijing Machi 4, 2026. (Xinhua/Shen Hong) BEIJING – Wajumbe wa Bunge la 14 la Umma la China (NPC) wamekusanyika Beijing jana Jumatano kwenye kikao cha maandalizi ya mkutano wa mwaka wa bunge hilo, ambapo wamechagua wajumbe wa tume ya utendaji wa mkutano wa mwaka na kupitisha ajenda za mkutano huo uliopangwa kuanza leo Alhamisi.