

Lugha Nyingine
Sanya, China: Mashindano ya Mashua ya Dragoni yafanyika kati ya ndege na mawimbi ya maji
Mashindano ya Wazi ya Mashua ya Dragoni ya Sanya 2025 yalifanyika kwa shamrashamra Mei 31 katika Mto Sanya, Mkoa wa Hainan, China, ambapo timu 18 za mashua ya Dragoni zilipiga makasia kwa kasi kushindana kwenye mto huo, ikiwasilisha tamasha la kuvutia linalochanganya ujadi na usasa, michezo na utamaduni.
"Nimeshiriki kwenye mashindano haya kwa miaka mingi, na Mto Sanya siku zote umekuwa safi sana. Mikoko katika pande zote hasa ni msitu mnene. Tunapopiga makasia kuongeza kasi ya mashua ya dragoni, miruko ya maji na sauti huwafanya ndege yangeyange waliojificha kwenye mikoko kuruka juu — wengine hata huruka sambamba na mashua ya dragoni kwa muda mfupi. Hali ya mapatano kati ya binadamu na mazingira ya asili hasa, ni yenye kuvutia sana!” amesema mmoja wa washiriki wa mashindano hayo.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma