

Lugha Nyingine
Marafiki wa Kimataifa washiriki Mashindano ya Mbio za Mashua ya Dragoni mjini Sanya, China
Tarehe 31, Mei ilikuwa Sikukuu ya Duanwu, sikukuu ya jadi ya China ambayo husherehekewa kwa mashindano ya mashua ya dragoni. Katika asubuhi ya siku hiyo, Charline, mpiga makasia wa Timu ya Kimataifa ya HelloSanya kutoka Ufaransa pamoja na wenzake walishiriki kwenye Mashindano ya Wazi ya Mbio za Mashua ya Dragoni ya Sanya 2025 yaliyofanyika mjini Sanya, Hainan, China, ambapo walijionea wenyewe uzuri wa utamaduni wa jadi wa China.
“Jadi hii (ya mbio za mashua ya dragoni) ni ya kuvutia sana, na cha muhimu zaidi ni kwamba, tumepata marafiki wapya wengi hapa,” anasema Charline kwa furaha.
Timu ya HelloSanya inaundwa na wachezaji kutoka zaidi ya nchi kumi, na kwa wastani wachezaji hao wamekuwa wakiishi Sanya kwa zaidi ya miaka mitatu, wengi wao wakijihusisha na mawasiliano ya kimataifa.
Kulikuwa na timu nyingine ya mashua ya dragon ya wachezaji wa kimataifa iliyoshiriki mashindano hayo siku hiyo, Timu ya Kimataifa ya Ulaya-Afrika-Asia, ambayo wapiga makasia wake pia wametoka zaidi ya nchi kumi za Ulaya, Afrika na Asia. Wamekutana na kujuana kupitia mashindano hayo.
Kabla ya mashindano kuanza, Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya Wazi ya Mbio za Mashua ya Dragon ya Sanya iliandaa darasa maalum la kujionea na kuufahamu utamaduni wa mashua ya Dragoni kwa wapiga makasia hao wa kigeni, ikiwawezesha kufahamu kwa kina mvuto wa kipekee wa utamaduni wa mashua ya dragoni kupitia maelezo ya kinadharia, uonyeshaji vitendo, na mbinu zingine.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma