Mradi mpya wa umeme wa nguvu ya juu waanza kusambaza umeme kutoka Xinjiang hadi Chongqing, China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 11, 2025
Mradi mpya wa umeme wa nguvu ya juu waanza kusambaza umeme kutoka Xinjiang hadi Chongqing, China
Picha hii ikionyesha mandhari ya sehemu ya Xinjiang ya mradi wa usambazaji umeme wa nguvu ya juu ya ±800 kV kwa mkondo wa moja kwa moja wa Hami-Chongqing, huko Hami, Mkoa unaojiendesha wa Xinjiang, kaskazini-magharibi mwa China, Oktoba 30, 2024. (Picha na Wu Shiping/Xinhua)

HAMI - Kampuni ya Gridi ya Kitaifa ya China imetangaza jana Jumanne kuanza kufanya kazi kwa mradi wa usambazaji umeme wa nguvu ya juu ya ±800 kV kwa mkondo wa moja kwa moja unaounganisha mji wa Hami wa mashariki mwa Mkoa wa Xinjiang na Mji wa Chongqing, kusini magharibi mwa China.

Hii inamaanisha kuwa mradi mkubwa wa tatu wa China kusambaza umeme kutoka mkoa wenye utajiri wa nishati wa Xinjiang hadi maeneo mengine ya nchini China.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha