人民网首页

Habari

Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing kuongeza uelewano na urafiki: Mabalozi

NEW YORK – Konsela mkuu wa ubalozi wa China katika Mji wa New York nchini Marekani Huang Ping amesema kwamba, Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing ya Mwaka 2022 siyo tu itaongeza maelewano na urafiki kati ya nchi na sehemu mbalimbali, lakini pia itaongeza imani na matumaini kwa binadamu kushirikiana katika kukabiliana na changamoto. Katika Makala yake iliyochapishwa wiki hii na Gazeti la Philadelphia Inquirer, Huang amewaalika wanamichezo kutoka Marekani na duniani kote kukusanyika pamoja mjini Beijing, kutimiza ndoto yao ya Olimpiki, kufahamu utamaduni wa China, na kusalia kumbukumbu zisizosahaulika za Olimpiki ya Majira ya Baridi maishani yao.

Kamati ya Michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi ya Beijing mwaka 2022 yachapisha kitabu cha kwanza cha mwongozo dhidi ya UVIKO-19

BEIJING – Toleo la kwanza la Kitabu kinachoelezea hatua za kupambana na UVIKO-19 kwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing mwaka 2022 kimetolewa leo Jumatatu. Kitabu hicho cha mwongozo, kilichochapishwa kwa pamoja na waandaaji wa Beijing 2022, Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC) na Kamati ya Kimataifa ya Michezo ya Olimpiki ya Walemavu (IPC) kinatoa matoleo tofauti kwa wanariadha na maafisa wa timu pamoja na wahusika wengine ikiwa ni pamoja na familia ya wanariadha, vyombo vya habari, Mashirikisho ya Kimataifa (IFs) na maafisa wa kiufundi.

Shughuli ya wakati wa siku 100 zinazobaki  kabla ya Michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi ya Beijing ya mwaka 2022 ilifanyika kwa shangwe Beijing tarehe 26, Oktoba.  Mjumbe wa kudumu wa Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya Chama, ambaye pia ni naibu waziri mkuu wa China na kiongozi wa kikundi cha uongozi wa kazi ya Michezo ya Olimpiki ya 24 ya majira ya baridi Bw. Han Zheng alishiriki kwenye shughuli hiyo, na kutangaza kutolewa kwa medali za Michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi ya Beijing “Tongxin” ambayo maana yake ya Kichina ni “kushirikiana kwa moyo mmoja ”.

Medali za Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi na Michezo ya Olimpiki ya Walemavu ya Majira ya Baridi ya Beijing 2022 Zatolewa

Shughuli ya wakati wa siku 100 zinazobaki kabla ya Michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi ya Beijing ya mwaka 2022 ilifanyika kwa shangwe Beijing tarehe 26, Oktoba. Mjumbe wa kudumu wa Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya Chama, ambaye pia ni naibu waziri mkuu wa China na kiongozi wa kikundi cha uongozi wa kazi ya Michezo ya Olimpiki ya 24 ya majira ya baridi Bw.

(Picha zinatoka tovuti ya Shirika la Habari la China Xinhua.)

Picha: Hafla ya kukaribisha moto wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijng 2022 yafanyika hapa Beijing

Leo asubuhi, moto wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing mwaka 2022 umefika hapa Beijing, na hafla ya kuukaribisha imefanyika kwa shangwe. Halafu, mpango wa kuonesha moto huo na wa kupokezana kwa mwenge ulitangazwa.

Iliyopita18 19 20 21 22 Inayofuata