Sikukuu ya Mashua ya Dragoni yasherehekewa kote China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 03, 2025
Sikukuu ya Mashua ya Dragoni yasherehekewa kote China
Mtoto akionyesha kazi ya sanaa yenye mchoro wa mashua ya dragoni juu yake katika Wilaya ya Tancheng, Mji wa Linyi, Mkoa wa Shandong, mashariki mwa China, Mei 31, 2025. (Picha na Zhang Chunlei/Xinhua)

Sikukuu ya Mashua ya Dragoni, ambayo pia inajulikana kwa jina la Sikukuu ya Duanwu kwa Kichina, ni sikukuu ya jadi ya China kumkumbuka mshairi wa China ya kale Qu Yuan kutoka Enzi ya madola ya kivita (475-221). Ikiwa inasherehekewa siku ya tano ya mwezi wa tano kwa kalenda ya kilimo ya China, sikukuu hiyo, kwa mwaka huu iliangukia Mei 31 ambapo Wachina walikuwa na mapumziko ya siku tatu yaliyofikia tamamati jana Jumatatu. 

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha