人民网首页
Picha hii ya angani iliyopigwa Aprili 26, 2023 ikionyesha eneo la ujenzi wa Reli Kiunganishi ya Pwani ya Mashariki (ECRL), mradi mkubwa wa miundombinu chini ya Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja (BRI) mjini Kelantan, Malaysia. (Xinhua/Zhu Wei)

BRI yaleta muunganisho ulioimarishwa kwa maendeleo na ustawi wa pamoja: wataalam

KUALA LUMPUR – Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja (BRI) lililotolewa na China limesonga mbele muongo mmoja tangu kuzinduliwa kwake na linaendelea kukua katika wigo na kiwango, na kuleta muunganisho bora wa miundombinu kwa maendeleo na ustawi wa pamoja, wataalam wamesema kwenye kongamano la kimataifa lililofanyika Kuala Lumpur, Malaysia. Kwenye ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa la Asia Mpya Jumuishi (IFNIA) 2023 siku ya Jumatatu, Ong Tee Keat, Mkuu wa Taasisi ya Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja ya Asia Pasifiki ametoahotuba akisifu mafanikio madhubuti yaliyofikiwa na BRI katika muongo mmoja uliopita.…

Wasafiri wanaoelekea ng'ambo wakipanda basi la abiria kwenye Kivuko cha Khunjerab katika Eneo linalojiendesha la Kabila la Watajik la Taxkorgan, Mkoa unaojiendesha wa Xinjiang, Kaskazini-Magharibi mwa China, Novemba 6, 2023. (Xinhua/Ding Lei)

Kivuko cha Khunjerab, bandari kuu ya nchi kavu inayounganisha China na Pakistan

Kikiwa kinapatikana katika Eneo linalojiendesha la Kabila la Watajik la Taxkorgan, Mkoa unaojiendesha wa Xinjiang, Kaskazini-Magharibi mwa China, Kivuko cha Khunjerab ni bandari kuu ya nchi kavu kwenye mpaka wa China na Pakistani, kituo kikuu cha biashara kati ya China na Pakistani, na lango muhimu la kuingia Asia Kusini na Ulaya. Tangu kuanza upya kwa utoaji vibali vya forodha kwa abiria Mwezi Aprili 3, 2023, Kivuko cha Khunjerab kimerekodi abiria zaidi ya 40,000 wanaoingia na kutoka.…

Balozi wa China nchini Tanzania, Chen Mingjian (wa pili kulia) akitoa taarifa ya matokeo ya Mkutano wa Baraza la Tatu la Ushirikiano wa Kimataifa wa Ukanda Mmoja, Njia Moja uliofanyika Beijing, China wiki iliyopita wakati wa mkutano na wanahabari jijini Dar es Salaam, Tanzania, Oktoba 26, 2023. (Xinhua/ Li Yahui)

China yaahidi kuhimiza ushirikiano wa Ukanda Mmoja, Njia Moja na Tanzania

DAR ES SALAAM - Balozi wa China nchini Tanzania, Chen Mingjian, amesema China inatarajia kuendelea kuhimiza ushirikiano wa Ukanda Mmoja, Njia Moja na Tanzania, ili kwa pamoja kuendeleza mustakabali mzuri wa baadaye wa maendeleo ya kisasa. Balozi Chen ameyasema hayo kwenye mkutano na wanahabari jijini Dar es Salaam, Tanzania, ambapo aliwasilisha taarifa ya matokeo ya Mkutano wa Baraza la Tatu la Ushirikiano wa Kimataifa wa Ukanda Mmoja, Njia Moja uliofanyika Beijing, China uliofanyika Beijing, China wiki iliyopita.…